Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kukitangaza vya kutosha Kivutio cha Maporomoko ya Maji Rusumo ili kuchangia pato la Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana ninalo swali moja la nyongeza. Kwanza, niishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri ya kutia moyo. Kwa kuwa umekiri kuwepo kwa maporomoko hayo ambayo ni kivutio lakini yamepotea baada ya uchepushaji kwenye mradi wa umeme Rusumo. Je, huoni sasa ipo haja kupitia Wizara yako na Wizara ya Nishati mshirikiane kurejesha maporomoko hayo yawe kama awali ili yaendelee kuwa kivutio katika Wilaya yetu ya Ngara?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Semguruka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Ngara kwa kushirikiana na kampuni ya umeme ambayo itapewa jukumu la kuendesha mradi ule wa umeme pale Rusumo tayari wanamkakati wa kupanda miti katika eneo lote lile la ukanda wa mradi ule, ni imani yetu kwamba baada ya kufanyika upandaji wa miti ule hali ya upatikanaji wa maji katika eneo lile itaimarika na hivyo uwezekano mkubwa wa kivutio hiki kuendelea kutumika.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kukitangaza vya kutosha Kivutio cha Maporomoko ya Maji Rusumo ili kuchangia pato la Taifa?

Supplementary Question 2

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kutoa ajira kwa mkataba wa muda mfupi kwa askari wa VGS ilikuweza kupunguza tatizo kubwa ama uhaba wa askari wa wanyama pori nchini? (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inao mkakati wa kuhakikisha kwamba pale ambapo mafunzo ya askari wa vijiji yamefanyika na kumekuwa na uhitaji wa askari hawa kupatiwa ajira, tunashirikiana na halmashauri kuona jinsi ambavyo kupitia miradi mbalimbali tulioyonayo akari hawa badala ya kupewa ajira wanaanzishiwa miradi itakayowaingizia kipato ili wakati wakifanya shughuli hii ya uhifadhi lakini vilevile waweze kujiongezea kipato.

Mheshimiwa Spika, tumeanza zoezi hilo kwa mradi wa REGROW ambao unajielekeza kwenye kufungua fursa za utalii katika mikoa ya Kusini tunaamini mafunzo tutakayoyapata kutokana na mradi huu yatatuonesha ni jinsi gani tunaweza kuendeleza katika maeneo mengine.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kukitangaza vya kutosha Kivutio cha Maporomoko ya Maji Rusumo ili kuchangia pato la Taifa?

Supplementary Question 3

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, kwa kuwa kivutio chetu pekee cha maporomoko ya Rusumo sasa kimepunguza mvuto baada ya uwekezaji wa mradi wa umeme pale Rusumo, Serikali haioni kuna haja sasa ya kuisaidia Ngara kuendeleza vivutio vingine ili Ngara isiondoke kwenye ramani ya kupata watalii, ahsante sana.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kivutio cha Rusumo siyo kivutio pekee kilichopo katika ukanda huu tunazo mbuga za wanyama zilizoko katika ukanda huu. Vilevile, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi tunaangalia kutumia uwepo wa mradi wa umeme kuufanya kama sehemu ya kivutio. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kuendeleza utalii katika ukanda huu tutaunganisha vivutio vingine vyote vilivyopo ili Sekta ya Utalii iweze kunufaisha ukanda huu na nchi yetu kwa ujumla.