Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:- Je, upi mpango wa kuboresha Vituo vya Polisi Busanda hususani Kituo cha Katoro na Chigunda?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali kwamba kuna fedha imetengwa. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, uboreshaji wa vituo hivi ulihitaji vile vile uongezaji wa idadi wa askari. Nini kauli ya Serikali juu ya uongezaji wa askari kwenye vituo hivi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Uboreshaji wa vituo hivi vile vile ulihitaji kujenga nyumba za askari kwenye maeneo ya vituo hivi. Nini kauli ya Serikali kwenye ujenzi wa nyumba hizo? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bryceson Magessa, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la upungufu wa askari, hivi karibuni tunaendelea na mchakato wa kuajiri askari wapya. Wako askari ambao wanakamilisha mafunzo yao hivi karibuni na wengine tumetangaza hivi karibuni askari wapya. Kwa hiyo, miongoni mwa askari hao watakapomaliza mafunzo yao tutawapeleka ili kukabiliana na upungufu wa askari kwenye maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, halikadhalika tunatambua pia changamoto ya makazi ya askari katika maeneo hayo. Namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira tukikamilisha ukarabati katika bajeti ijayo tutaangalia vile vile uwezekano wa kutatua changamoto au kupunguza changamoto ya makazi ya askari katika eneo hilo.