Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Serikali imeweka alama ya “X” ya kijani na nyekundu katika nyumba za wakazi wa Jimbo la Njombe Mjini kikiwemo na Kituo cha Polisi cha Njombe. Je, Serikali inasema nini juu ya tafsiri sahihi ya alama hizo?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri, kwa kuwa suala hili linawagusa karibu Watanzania wote na mimi nitajitahidi kwenda polepole kama alivyoenda yeye polepole. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nyumba nyingi…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwalongo naomba usiende polepole kwa sababu muda wetu unakimbia sana na watu wana maswali mengi. (Makofi/Kicheko)
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nyumba nyingi katika Mji wa Njombe zimewekewa alama ya kijani. Serikali haioni ipo haja ya sasa kufuta alama hizo ili kuwapa fursa wananchi wamiliki wa nyumba hizo kufanya ukarabati wa nyumba zao na kuzitumia nyumba zao kama dhamana katika taasisi za fedha? (Makofi)
Swali la pili, je, Serikali haioni sasa upo ulazima kuleta Sheria Namba 13 ya mwaka 2007 tuifanyie marekebisho ili ibainike bayana kwamba, maeneo ya mjini yawe na upana wa mita 42 badala ya 60 za sasa. Hii itasaidia kutunza historia za miji katika nchi yetu, lakini vilevile itaipunguzia gharama Serikali pamoja na wananchi? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumeweka „X‟ ya kijani kama ishara kwamba hilo eneo haliruhusiwi kuendelezwa, haliruhusiwi kujengwa nyumba mpya kwa sababu ni eneo la hifadhi ya barabara kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2007. Kwa hiyo, kusema wafute na ianze kutumika kama dhamana siyo sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Watanzania wote wakati tunapitisha sheria hii tulikuwa na malengo ya kuiendeleza nchi yetu kimiundominu, tupate fursa ya kupanua barabara na hatimaye zitupeleke katika karne ya viwanda, tuwe na maendeleo makubwa na huko ndiyo tunakoenda hatuwezi kurudi nyuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, suala la kubadilisha sheria, kwanza mimi binafsi na niliongea na Mheshimiwa Waziri wangu naongea kwa niaba yake kwa kweli tulitaka tupanue zaidi kwa sababu sasa hivi tunaenda kwenye miundombinu, sehemu za mijini kuna flyovers na highways lazima tuwe nazo ambazo zinahitaji ardhi kubwa zaidi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naibu Spika kama ifuatavyo:- (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, alama ya kijani ama nyekundu, maana yake nyumba hiyo haitakiwi kuwepo hapo kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2007. Tunachotaka, wale ambao walijenga kabla ya mwaka 2007 haki yao inayoongelewa hapa ni ya kufidiwa, siyo kuendelea kukaa, ila hatuwaondoi mapema mpaka pale tutakapokuwa na mahitaji ndipo tutakapowafidia. Ila tutakachokifidia ni kile kilichofanyika kabla ya mwaka 2007. Chochote kitakachokuwa kimefanyika baada ya mwaka 2007 kitabomolewa bila fidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja hiyo ya kubadilisha sheria mimi binafsi siiungi mkono lakini tumechukua ombi lako na tutaliwasilisha Serikalini likajadiliwe ili maamuzi ya Kiserikali yatolewe.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri watu wengi wamesimama, lakini nadhani swali la msingi hapo ni kwamba hawa watu wenye kijani umesema mpaka mtakapohitaji barabara. Kama jibu ni hilo, hawa watu waendelee kusubiri? Kama utaihitaji barabara baada ya miaka kumi, wao inabidi waendelee kusubiri wasifanye chochote kwenye hayo maeneo yao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naibu Spika kama ifuatavyo:- (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, alama ya kijani ama nyekundu, maana yake nyumba hiyo haitakiwi kuwepo hapo kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2007. Tunachotaka, wale ambao walijenga kabla ya mwaka 2007 haki yao inayoongelewa hapa ni ya kufidiwa, siyo kuendelea kukaa, ila hatuwaondoi mapema mpaka pale tutakapokuwa na mahitaji ndipo tutakapowafidia. Ila tutakachokifidia ni kile kilichofanyika kabla ya mwaka 2007. Chochote kitakachokuwa kimefanyika baada ya mwaka 2007 kitabomolewa bila fidia.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, kabla hujatoka, alama nyekundu ni kwamba wale watu wanatakiwa kubomoa wasiwepo; alama ya kijani maana yake sheria imewakuta. Sasa ndiyo anauliza Mheshimiwa Mwalongo wanatakiwa kusubiri muda gani hao wenye alama ya kijani ambao sheria imewakuta?
Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. (Makofi)
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hii alama ya kijani, hili tutalichukua na tutaliangalia tuone tutafanyaje.