Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wenye viwanda vilivyokufa au havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Famili kilichopo Salasala katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu aliyoyatoa, nina maswali mawili ya nyongeza.

Ningependa nimwambie Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba kule Njombe tuna Kiwanda cha Maziwa ambacho kimefungwa kwa muda mrefu na kiwanda kile kina wadau mbalimbali ambao wanahusika na kina changamoto nyingi sana.

Swali la kwanza je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuniambia Wizara hii ambayo kazi yake ni uratibu; je, anaweza sasa kuchukua hilo jukumu la kufanya uratibu ili wadau mbalimbali wa kiwanda kile waweze kukutana na kutatua hizo changamoto?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri anaweza kutoa commitment hapa sasa kwamba yeye pamoja na hao wadau watakuja Njombe ili kukaa na wakulima ambao wanaumia sana kutokana na kiwanda kile kutokufanyakazi? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deodatus Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Deodatus Mwanyika kwa kufuatilia sana kuhusiana na viwanda katika Mkoa wa Njomba na hasa Kiwanda hiki cha Maziwa ambacho muda mwingi anafuatilia.

Mheshimiwa Spika, ni kweli viwanda vingi havifanyikazi kutokana na changamoto mbalimbali na Serikali kama nilivyosema kupitia mpango wa kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara tunapitia mojawapo ni kuhakikisha tunatatua changamoto zinazokabili viwanda hivyo, ikiwemo kiwanda hiki cha maziwa cha Njombe; tutafanya tathmini tuone nini changamoto zilizowasibu mpaka kisiwe kinafanyakazi hivi sasa na hatimaye Serikali tutachukua hatua.

Mheshimiwa Spika, la pili; kwa sababu kweli kiwanda kinahusisha sekta tatu kwa maana ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara lakini tutashirikiana na wenzetu Wizara ya Kilimo, lakini Mifugo na Uvuvi ili tuweze kukitembelea kama nilivyosema kubaini changamoto ambazo zinazikabili kiwanda hiki ambacho kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge hakifanyikazi. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wenye viwanda vilivyokufa au havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Famili kilichopo Salasala katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza katika Wizara hii ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara.

Kwa muda mrefu Serikali kupitia TPDC imetenga eneo la kujenga Kiwanda cha Mbolea Kilwa Masoko itakayotokana na malighafi ya gesi asilia; na kwa mara ya mwisho tumepewa taarifa kwamba Serikali iko katika mazungumzo na mwekezaji.

Swali; mazungumzo kati ya Serikali na mwekezaji yamefikia hatua gani? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Ally kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli adhma ya Serikali ni kuona tunajitosheleza katika uzalishaji au mahitaji ya mbolea nchini ambayo ni takribani ya tani 700,000. Uzalishaji tulionao sasa si zaidi ya tani 100,000. Lakini mipango hiyo pamoja na mingine ni kuona gesi asilia katika Mkoa wa Mtwara inatumika kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema na TPDC kweli kuna eneo limetengwa na kwa kweli kama nilivyosema swali hapa Bungeni kuna wawekezaji wameshajitokeza ambao watakuja kuwekeza katika viwanda vya kuzalisha mbolea kwa kutumia gesi asilia.

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie Mbunge kwamba Serikali inafuatilia sana jambo hili ili kuhakikisha majadiliano hayo yanakamilika mara moja na kwa kweli tunafanya majadiliano kwa ajili ya kuona namna ya kuwavutia. Kwa sababu kilichopo hapa ni namna ya kuwavutia ili waweze kuwekeza katika kutumia gesi hiyo ikiwemo pamoja na mambo ya bei na mambo mengine/vivutio maalum ambavyo wanahitaji wawekezaji hao. Kwa hiyo, tutakamilisha na kuanza kuzalisha mbolea kupitia gesi asilia, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wenye viwanda vilivyokufa au havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Famili kilichopo Salasala katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 3

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwenye Jimbo langu la Nachingwea kuna viwanda viwili ambavyo kwa muda mrefu havifanyikazi; Kiwanda cha Lindi Pharmacy lakini pia Kiwanda cha Mafuta Ilulu.

Nini mpango wa Serikali kufufua viwanda hivi ili viweze kuzalisha ajira kwa vijana wetu? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Nachingwea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali kupitia ubinafsishaji tulibinafsisha viwanda 156 lakini katika viwanda hivyo viwanda 88 ndiyo vinafanyakazi vizuri, 68 vilikuwa havifanyikazi vizuri na moja ya maeneo ambayo tumekwishayafanyia kazi ni kuvirudisha baadhi ya viwanda ambavyo vipo 20, mojawapo vikiwa hivi viwanda viwili ambavyo alivitaja Mheshimiwa Mbunge, Kiwanda cha Mafuta Ilulu na kile kingine cha kubangua korosho cha Nachingwea.

Mheshimiwa Spika, lakini katika hatua za awali tumeshafanya tathmini viwanda hivi ni kati ya viwanda ambavyo tutaviweka katika maeneo ya uwekezaji kwa ajili ya kuzalisha bidhaa kwa ajili ya mauzo nje (SEZ).

Kwa hiyo, tayari tumeshachukua hatua mbalimbali na sasa tunaendelea kutafuta wawekezaji ambao tutashirikiana nao, ili wazalishe bidhaa aidha za mafuta au kubangua korosho kama ilivyokuwa awali kwa ajili ya kuuza nje. Kwa hiyo, tayari tumeshachukua hatua kwamba hivi vitakuwa chini ya maeneo huru ya uwekezaji kwa ajili ya mauzo nje na hivi viwanda vitafufuliwa tutakapopata mwekezaji mapema iwezekanavyo. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wenye viwanda vilivyokufa au havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Famili kilichopo Salasala katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 4

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi; masuala ya uwekezaji wa viwanda si tu yanaleta tija kubwa kwenye ajira na kusaidia upatikanaji wa bidhaa kwenye soko la ndani yakiwemo mafuta ya kupikia na bidhaa nyingine.

Nini mkakati wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha kuisaidia Benki ya Rasilimali Tanzania (Tanzania Investment Bank Development) kupata mitaji ya uhakika kwa ajili ya viwanda? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli azma ya Serikali ni kuona namna gani tunawasaidia wawekezaji hasa wa ndani kupitia kuwasaidia kwenye changamoto ya mitaji ya rasilimali fedha. Kwa hiyo, mojawapo ni kupitia mabenki yetu yanayosaidia wawekezaji ikiwemo Benki hii ya Rasilimali na mabenki mengine. Lengo la Serikali ni kuhakikisha tunaweka mazingira wezeshi ikiwemo hiyo ya kuwapa mitaji au kuhakikisha wawekezaji ambao wanataka kuwekeza kwenye viwanda hivi wanapewa huduma hiyo ya kifedha.

Kwa hiyo, Serikali itaendelea kufanyakazi kuona kila namna inayowezekana kuwezesha benki zetu ambazo zinakopesha wafanyabiashara au wawekezaji katika sekta ya viwanda. Nakushukuru sana.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wenye viwanda vilivyokufa au havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Famili kilichopo Salasala katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 5

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pale Musoma Mjini tuna tatizo kubwa sana la ajira kwa sababu viwanda vingi vimekufa; vilikuwepo viwanda vya samaki vimekufa, Kiwanda cha Nguo cha MUTEX kimekufa, Kiwanda cha Maziwa kimekufa, Kiwanda cha Mkonge kimekufa. Sasa ni zaidi ya miaka kumi kila siku Serikali inaahidi kutafuta wawekezaji. Sasa tunapenda kujua, ni lini sasa itatusaidia kupata hawa wawekezaji ili watu wetu waendee kupata ajira? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, napenda kujibu swali la nyongeza dogo la Mheshimiwa Vedastus Manyinyi, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama nilivyosema, tulipofanya tathmini ya mwaka 2017 kuhusiana na viwanda vilivyobinafsishwa, viwanda vingi zaidi ya 68 vilikuwa havifanyikazi vikiwemo viwanda ambavyo viko katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge kule kule Musoma. Kama nilivyosema katika tathmini hiyo tumeshavigawa vingine tunavitafutia wawekezaji, lakini vingine tutaviweka katika mashirika maalum ikiwemo maeneo huru ya uzalishaji kwa ajili ya mauzo ya nje (SEZ), lakini vingine katika taasisi zetu kama Shirika la Maendeleo la Taifa – NDC na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, lakini katika kutafuta wawekezaji kuna hatua mbalimbali kwa sababu tusingependa kurudia tena makosa tuliyoyafanya huko nyuma kutafuta/kupata wawekezaji ambao siyo mahiri. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba Serikali inajitahidi kuhakikisha kuweka mazingira wezeshi, ili kuvutia wawekezaji ambao tunajua watakuwa ni makini na wenye nia thabiti ya kuvifufua au kujenga viwanda vingine ambavyo vitakuwa na tija kwa ajili ya maendeleo ya nchi hii. Nakushukuru sana.