Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH A. MRIMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka alama za mipaka katika Hifadhi ya Serengeti na Pori la Akiba la Ikorongo ili kumaliza migogoro na vijiji jirani?

Supplementary Question 1

MHE. JEREMIAH A. MRIMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuja kwa timu ya Mawaziri nane ambayo ilitangaza kuongezwa kwa eneo la mita 500 eneo la Kinga katika vijiji vya Mbilikili, Bisarara, Tamkeri, Mbalibali, Gwikongo, Machochwe, Nyamakendo pamoja na Meringa. Pia katika nyakati tofauti mwaka 2008, 2010, 2013 mipaka ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na vijiji hivyo imekuwa ikibadilishwa.

Sasa je, Waziri wa Maliasili pamoja na Waziri wa Ardhi wako tayari kuja Serengeti wakiambatana nami mapema iwezekanaavyo wakiwa na GN ya mwaka 1968 yenye ramani namba 14, 15, 4 ili kutatuza tatizo hili kwa sababu ni la muda mrefu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali namba mbili; mwaka 1994 Serikali ilipunguza eneo la Grumeti Game Reserve pamoja na Ikorongo Game Reserve kutoka kilometa za mraba 3,600 kuwa 993.4 lakini mpaka sasa kumbukumbu za Serikali bado hazijafanya mabadiliko hayo. Kwa hiyo, wananchi wa Makundusi, Pakinyigoti, Rwamchanga, Rwabando wamekuwa wakizuiwa kufanya shughuli zao. Je, ni lini mabadiliko hayo yatafanyika? Ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jeremiah Amsabi Mrimi, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mipaka kama ambavyo timu ya Mawaziri nane ilipita kutoa ufafanuzi, lakini pia ikaacha watumishi ambao walikuwa wanafanya tathmini ya namna ya kuja kutoa ufafanuzi juu ya mipaka hiyo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Serengeti na wananchi wa Serengeti kwamba tathmini sasa hivi imeshakamilika na kinachofuata sasa ni kwenda kuonesha mipaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Wizara ya Maliasili na Utalii tukishirikana na wizara ya Ardhi tutaenda kufafanua hii mipaka tukiwa na wananchi wa maeneo hayo na lengo ni kuondoa sasa ile vurugu au taharuki ya kutotambua mipaka kati ya hifadhi na wananchi.

Kwa hiyo, niwahakikishie hawa wananchi kwamba tathmini imeshakamilika tunakuja sasa kufafanua utambuzi wa mipaka ni ipi ya hifadhi ni ipi ya wananchi, hilo linaenda kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na swali lake la pili limehusiana na ufafanuzi wa GN baada ya kurekebishwa eneo la Hifadhi ya Ikorongo; Serikali italifanyia kazi eneo hili na tutapeleka waraka kwa wananchi kwa maandishi sasa kuonesha kwamba eneo hili litakuwa ni la hifadhi na lile ambalo limeachwa kwa wananchi ili wawe na uwezo sasa wa kufanya shughuli zao za kila siku, tutaenda kulifanyia kazi na tutatoa taarifa kwa wananchi wa Wilaya ya Serengeti.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JEREMIAH A. MRIMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka alama za mipaka katika Hifadhi ya Serengeti na Pori la Akiba la Ikorongo ili kumaliza migogoro na vijiji jirani?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Waziri kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu sana kati ya Hifadhi ya Kitulo na Vijiji vya Misilo, Lugoda, Igenge, Nkindo na Makwalanga. Je, lini Serikali itamaliza tatizo hili la mipaka kati ya Hifadhi na vijiji hivi? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Neema, Mbuge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwape pole wananchi wa Makete hususan wanaozunguka eneo hili la Kitulo. Nilishawahi kuzungumza na Mheshimiwa Mbunge na nikatoa ahadi kwamba tungeenda kuutatua huu mgogoro, lakini kutokana na changamoto mbalimbali sikuweza kupata huo muda. Lakini ninamuahidi Mbunge na ananitazama hapa kwamba wananchi wa Makete wakae mkao wa kusubiri, tunaenda na Mheshimiwa Mbunge kutatua mgogoro huu. Na mgogoro huu tunaenda kuumaliza ili wananchi waweze kufanya kazi kwa uhuru na hifadhi tuweze kuisimamia vizuri. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. JEREMIAH A. MRIMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka alama za mipaka katika Hifadhi ya Serengeti na Pori la Akiba la Ikorongo ili kumaliza migogoro na vijiji jirani?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza nalo liko hivi; je ni lini Serikali itatua mgogoro kati ya Arusha National Park na wananchi wa Kijiji cha Lukungw’ado ambao unatokana na Serikali haikununua bila kushirikisha Serikali ya Kijiji mashamba Namba 40 na Namba 41 ambayo wananchi walikuwa wanategemea kujikimu nakushukuru sana.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza na Mheshimiwa Pallangyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti suala la kutatua migogoro ni wajibu wa Wizara ya yale maeneo ambayo hatujayafikia ni mhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakuja kuyatatua, na ukizingatia maeneo mengi yalikuwa kwenye vijiji 920, lakini kwa yale maeneo ambayo hayakuingizwa kwenye vile vijiji 920, na migogoro yao ni mipya tumeshaelekeza wananchi kupitia wawakilishi wao watuletee malalamiko haya ili tupite katika maeneo hayo tuweze kutatua migogoro hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro mingine ni ya kufika sisi kama viongozi, kukaa na wananchi tukaisikiliza. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaambatana katika Jimbo lake ili tuweze kutatua mgogoro huu.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JEREMIAH A. MRIMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka alama za mipaka katika Hifadhi ya Serengeti na Pori la Akiba la Ikorongo ili kumaliza migogoro na vijiji jirani?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; migogoro ya ardhi kati ya Hifadhi ya Serengeti Wilaya ya Serengeti na Wilaya ya Tarime, Bunda umekuwa ni wa muda mrefu na ambao mingine inapelekea hata kuzuia wananchi kufanya shughuli zao, mathalani Kata ya Nyatwali iliyopo Wilaya ya Bunda ambayo ina vijiji vitatu, cha Serengeti, Tamahu na Nyatwali yenyewe ina wakazi takribani 10,000 na Serikali imepeleka miradi ya umwagiliaji takribani wa bilioni 1.7 na maji safi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakazi hao wamezuiliwa kuendeleza makazi yao takribani miaka 10; tunataka kujua ni kwa nini Serikali isiwaache hao wananchi waendeleze na makazi kwa sababu mmeshindwa kuwalipa fidia ili iweze kuondoka takribani miaka 10 sasa hivi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna maeneo mengo likiwemo eneo la Nyatwali ambalo kiuhalisia lilikuwa ni eneo la wananchi, na nipende tu kuwaambia wananchi wa Nyatwali kwamba hakuna mgogoro isipokuwa wananchi walioko pale wako kihalali kabisa, wanaishi kihalali na Serikali ilishasajili vijiji na wananchi wapo miaka ya tangu 1974, wapo pale. Hilo niwaondoe wasiwasi, hakuna mgogoro isipokuwa yale maeneo hata wewe ni shahidi umekuwa ukiona malalamiko mengi ya Waheshimiwa Wabunge wananchi wao wanalalamika kwamba kwa asilimia kubwa wanachangamoto ya wanyama wakali hususani tembo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hili wananchi wa Nyatwali ni mojawapo ya maeneo ambayo yana kilio hiki, tathmini ya Serikali ni kuangalia namna iliyobora ya kuepusha hawa wananchi wasiendelee kuteseka na wanyama wakali. Maeneo ni mengi yamezibwa yamewekwa makazi ya kudumu, wananchi wamejenga kwenye maeneo ambayo ni mapito ya wanyama ukiangalia eneo la Nyatwali ni eneo moja wapo ambalo upande mmoja ni Serengeti National Park, upande mwingine ndio Nyatwali ilipo na vijiji vya jirani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiruhusu pale wananchi kuendelea kuishi changamoto ya wanyama wakali tutaendelea kulia kila siku kwa hiyo mimi niwaombe wananchi, maeneo yote ambayo tumeyainisha Serikali imesitisha kuleta huduma mbalimbali, Serikali imeshaanza kufanya tathmini wananchi watalipwa kupisha maeneo hayo. Na hili ni tamko la Serikali kwamba ili kupunguza athari za wanyama wakali ni vyema tukatafuta eneo maalum ya mapito ya wanyama kuliachia ili wananchi waishi kwa amani na wanyama waendelee kupita katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili tunalishughulikia kwa uhakika na kwa haraka zaidi ili wananchi waweze kuishi kwa amani na Serikali iendelee na taratibu za uhifadhi ahsante.