Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Manyara?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nichukue nafasi hii kuishukuru Serikali kwa kutengwa kwa kiwango hicho cha fedha na mwezi Oktoba jengo hilo litakuwa limekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la nyongeza; kwa kuwa kwa sasa Mkoa wetu wa Manyara tuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa hati za kusafiria lakini pamoja na hati za makazi. Inatulazimu kupata huduma hiyo Mkoa wa Arusha, Mkoa wa Dodoma na Mkoa wa Singida na siyo Mkoa wa Manyara.

Je, Serikali iko tayari sasa kutufungia elektroniki ili tuweze kupata huduma hiyo ndani ya Mkoa wetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili; kwa kuwa Mkoa wa Manyara uko pembezoni na wahamiaji haramu wengi wanatumia kama njia ya kupita kwenda kwenye nchi zingine.

Je, Serikali haioni haja ya kutuongezea watumishi pamoja na usafiri kwa sababu kwa sasa watumishi wetu wanatumia pikipiki badala ya usafiri wa magari?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Halamga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakiri kwamba katika Mkoa wa Manyara huduma za kutoa pass kwa electronics zilikuwa hazijafungwa kwenye jengo hili kwa sababu jengo lilikuwa halijakamilika. Hivi sasa watumishi wa ngazi ya Mkoa wako kwenye jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara na mimi nimshukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kuwaweka watumishi hawa kwenye jengo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini namuahidi Mheshimiwa Halamga, jengo litakapokamilika mifumo yote ya electronic ya utoaji wa pass zitatolewa kwenye jengo letu la uhamiaji baada ya Oktoba mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu nyongeza ya watumishi na magari, nakubali kwamba Mkao wa Manyara unalo gari moja tu aina ya Forde Ranger liliko ngazi ya Mkoa, Wilayani kule tunatumia usafiri wa pikipiki, lakini pia kuna uhaba wa watumishi kama alivyokwishaeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Waheshimiwa Wabunge wanakumbuka wakati wa bajeti tulitamka kwamba wapo watumishi 820 ambao wataajiriwa kama watumishi wapya, wako kwenye mafunzo sasa hivi, wanatarajia kuhitimu mwezi Septemba, 2022. Katika mpango wetu wa ugawaji tutazingatia maeneo yenye upungufu mkubwa zikiwemo Wilaya za Mkoa wa Manyara. Nashukuru.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Manyara?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililoko Manyara ni sawasawa na Halmashauri ya Msalala, Wilaya ya Kahama. Kwa kuwa Kata ya Isaka kumekuwa na ongezeko la wageni mbalimbali na ukizingatia uwepo wa bandari na uendelezaji wa ujenzi wa bandari mpya, hivyo kuongeza idadi ya watu katika Kata ya Isaka. Sasa Serikali ina mpango gani wa kuanzisha kituo cha uhamiaji?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi, Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua uwepo wa muingiliano mkubwa wa wananchi pamoja na wageni kwenye eneo lake hasa kutokana na shughuli kubwa za kiuchumi za uchimbaji wa madini na kwa mtaji huo ni halali Wilaya yake kupata ofisi ya uhamiaji. Na sera ya Wizara ni kuhakikisha kwamba kila ilipo wilaya siyo halmashauri na pale Wilaya ya Kahama ipo ofisi yetu ya Uhamiaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba watu wote wanaokwenda Msalala waendelee kutumia huduma zinazotolewa katika ofisi ya wilaya ambayo iko pale Kahama. Lakini patakapotokea umuhimu wa kupanua zile huduma kuzipeleka kule, tutashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kupata majengo kule ili yaweze kutumika kutoka huduma hiyo. Nashukuru.