Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Kituo cha Afya Mtina ili kiweze kutoa huduma ya upasuaji pamoja kupeleka vifaatiba katika Kituo cha Afya Mchoteka?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali; kwa kuwa Kituo cha Afya Mtina kinahudumia zaidi ya kata nne na changamoto ya kituo kile ni pamoja na kutokuwa na huduma ya upasuaji.

Je, Naibu Waziri anaweza kunihakikishia baada ya Bunge hili atembelee kituo kile ili aweze kuona changamoto za wananchi wa kata ile?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Jimbo la Tunduru Kusini lina kata 15, vituo vya afya vinavyopatikana mpaka sasa ni vitatu ambavyo vyote havituoi huduma ya upasuaji kutokana na tatizo la kutokuwa na vifaa vya upasuaji, lakini kwa kuwa tunahitaji vituo vya afya vingi.

Je, Serikali ina mpango gani ya kuongeza angalau vituo vya afya viwili katika Kata ya Malumba na Kata ya Msechela ambazo zipo mpakani mwa Msumbuji ili kutoa huduma kwa wananchi wale ambao wanahudumiwa kutoka mbali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Jumbo la Tunduru Kusini kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Kituo cha Afya cha Mtina, Serikali imeshatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la upasuaji. Kwa hiyo, katika mwaka ujao wa fedha tuna uhakika sasa changamoto hiyo tutakuwa tumeondokana nayo, lakini nipo tayari kuambatana na Mheshimiwa Mpakate kwenda kutembelea kituo cha afya hiki na vituo vingine katika Jimbo lake ili kuona utoaji wa huduma lakini pia kuweka mipango ya pamoja kuhakikisha tunaboresha huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na ujenzi wa vituo vya afya katika kata zake 15 tunachukua kata zake mbili na bahati njema Waheshimiwa Wabunge walileta kata tatu za kipaumbele na Serikali inapitia huko kuandaa mpango wa utekelezaji wa ujenzi wa vituo vya afya kwenye kata tatu za kipaumbele kwa kila jimbo. Kwa hiyo, tutafanya hivyo katika jimbo hili la Tunduru Kusini. Ahsante.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Kituo cha Afya Mtina ili kiweze kutoa huduma ya upasuaji pamoja kupeleka vifaatiba katika Kituo cha Afya Mchoteka?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Katika Jimbo la Kilwa Kaskazini Serikali ikishirikiana na taasisi ya Pan African ilijenga kituo cha afya katika Kata ya Somanga, lakini kituo kile kimekuwa na changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa vifaatiba.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka vifaatiba ili huduma bora ya afya iweze kutolewa katika Kata ya Somanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WA ZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ametenga shilingi bilioni 69.95 mwaka ujao wa fedha kwaajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwenye vituo vya afya na hospitali za halmashauri. Kwa hiyo, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge akiwemo Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa Kaskazini kwamba kituo hiki cha afya ni miongoni mwa vituo ambavyo vitapelekewa vifaa tiba pamoja na vituo vingine vilivyokamilika ili viweze kuanza kutoa huduma za afya. Ahsante.