Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Viwanda vya Mbolea nchini ili Wakulima waongeze tija?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini kuna maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa sasa tunakaribia kwenda kusaini mkataba mkubwa wa uchakataji wa gesi asilia wa LNG kule Kusini na sehemu ya uzalishaji wa malighafi za gesi kuwa pia inatengeneza mbolea.

Je, ni upi mkakati wa Serikali kufungamanisha uchakataji wa gesi asilia na uanzishaji wa Kiwanda cha Mbolea katika eneo la Kusini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Mkoa wa Tanga ndiyo tutakaopokea hifadhi ya mafuta ghafi kutoka Uganda.

Je, Serikali haioni kwamba tunaweza tukatumia eneo la Chongoleani ikiwa ni sehemu pia ya usafishaji ghafi; kwa sababu mafuta haya pia ni malighafi kwa ajili kutengeneza mbolea tukapata Kiwanda kingine cha Mbolea katika Mkoa wa Tanga kama kile kilichokuwepo miaka ya nyuma? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Shangazi kwa kufuatilia maendeleo ya ujenzi wa viwanda hasa vya mbolea katika nchi hii na hasa katika Mkoa wa Tanga. Serikali ina mpango wa matumizi ya gesi asilia ambao unatekelezwa kupita Shirika letu la Maendeleo la Petroli (TPDC) lakini pia kwa kushirikiana na Kituo chetu cha Uwekezaji cha (TIC). Kwa hiyo, katika mpango huo tumeshaendelea kuvutia wawekezaji na zaidi ya kampuni tatu ambazo zimeonesha utayari wa kuwekeza katika kuzalisha mbolea kwa kutumia gesi asilia kampuni hizo ni pamoja na Helmik na Ferosta kutoka Ujerumani lakini pia tunayo Polyserve kutoka Misri, lakini zaidi na wengine wanaendelea kufanya tathmini na namna ya kutumia gesi asilia ikiwemo Kampuni ya Dangote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, katika mpango huo tumeshaendelea kuvutia wawekezaji, na zaidi ya kampuni tatu zimeonesha utayari wa kuwekeza katika uzalishaji wa mbolea kwa kutumia gesi asilia. Kampuni hizo ni pamoja na Helium na Feroster kutoka Ujerumani na pia tunayo Polysafe kutoka Misri. Vile vile na wengine wanaendelea kufanya tathmini ya namna ya kutumia gesi asilia ikiwemo Kampuni ya Dangote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni sahihi kabisa, ni mawazo mazuri kuona namna gani Tanzania inatumia fursa ya mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda ambayo yatakuja Tanzania, tuone namna gani ya kutumia mafuta hayo ghafi kuzalisha mbolea ili tukidhi mahitaji makubwa ya nchi hii kutokana na upungu au nakisi ya mbolea kwa ajili ya sekta ya Kilimo. Nashukuru. (Makofi)

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Viwanda vya Mbolea nchini ili Wakulima waongeze tija?

Supplementary Question 2

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa changamoto ya mbolea bado ni kubwa sana nchini; na kwa kuwa Tanga tulikuwa na Kiwanda cha Mbolea na sasa hivi hakifanyi kazi: Je, Serikali haioni haja sasa yakutafuta mwekezaji kwa ajili ya kwenda kuwekeza kwenye kiwanda kile ili kutatua changamoto kubwa ya mbolea tuliyonayo? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zodo, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama nilivyosema tuna changamoto kubwa sana ya mbolea, zaidi ya tani 600,000 zinahitajika katika kukamilisha mahitaji ya tani 700,000 kwa mwaka ambazo zinatumika katika nchi hii. Kwa hiyo, Serikali ina mpango wa kuendelea kufufua viwanda ikiwemo na hiki ambacho anasema Mheshimiwa Mbunge kule Tanga. Tutaona namna ya kutafuta wawekezaji ili waweze kuwekeza katika kiwanda hicho ili kuendelea kuzalisha mbolea kama ilivyokuwa hapo awali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Viwanda vya Mbolea nchini ili Wakulima waongeze tija?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi sana kununua viuatilifu hasa vinavyotumika katika zao la korosho, na mnunuzi mkubwa ni maeneo yote ya Mtwara na Lindi: Je, Serikali haioni sasa ni wakati muhimu wa kujenga viwanda vya viuatilifu ambavyo vinaendana na material hii ya gesi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchungahela Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna changamoto kama ilivyo kwenye mbolea, lakini pia kwenye viuatilifu ambavyo kwa kiasi kikubwa tunaingiza kutoka nje. Serikali imeshaanza mipango hiyo ikiwemo kuzalisha kupitia kile kiwanda chetu cha viuwadudu pale Kibaha, lakini tutaona pia namna ya kutumia gesi kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, ambapo nayo ikianza kuchakatwa inaweza kuzalisha viuatilifu mbalimbali ambavyo vinaweza kutumika katika sekta hii ya kilimo hasa kwenye mikorosho na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Viwanda vya Mbolea nchini ili Wakulima waongeze tija?

Supplementary Question 4

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kiwanda cha LOSAA, kiwanda ambacho ni cha ufundi wa ufumaji na Seremala; kilisimama kwenye ujenzi wake tangu mwaka 1973. Tukazungumza na Mheshimiwa Waziri akamtuma Katibu Mkuu wa Wizara yako, ametembelea pale na akaahidi kiwanda kile kitamaliziwa na kuanza kufanya kazi: Je, ni lini Serikali itaanza umaliziaji wa kiwanda hiki?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali tuna mpango wa kufufua viwanda vyote ikiwemo kiwanda ambacho anakisema Mheshimiwa Mbunge. Kweli Serikali tumeshachukua jitihada ikiwemo kutuma wataalamu wetu na Katibu Mkuu alishaenda pale kuweka tathmini ya kuona mahitaji halisi ya gharama ya kukiendeleza kiwanda kile.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali katika fedha za mwaka huu ambazo zimepitishwa hapa, mojawapo tutaangalia namna ya kuanza hatua za awali kukifufua kiwanda hicho ili kiweze kuendelea kufanya kazi na wananchi wa Jimbo la Hai weweze kunufaika na nchi nzima tuweze kutapa faida ya uwekezaji katika viwanda vyetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Viwanda vya Mbolea nchini ili Wakulima waongeze tija?

Supplementary Question 5

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali ya nyongeza. Kwa kuwa tafiti zimeonesha kwamba Gypsam au jasi inatoa mbolea ikichakatwa na kwa kuwa Wilaya ya Same ina jasi nyingi katika Kata ya Bendera na Makanya: Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka viwanda katika sehemu hizo? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kaboyoka, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika malighafi ambazo zinatumika katika kuzalisha mbolea, mojawapo ni Gypsam, na kwa sababu Mheshimiwa Mbunge amesema kuhusiana na Jimboni kwake, Mkoani huko, basi tutaona namna gani ya kuvutia pia wawekezaji waweze kuona namna ya kutumia malighafi zilizopo pale ili kuanzisha viwanda vya mbolea kama ambavyo tunavutia maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.