Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, ni vijana wangapi wamepata nafasi za masomo nje ya nchi kwa mwaka 2015 - 2020 na kati yao ni wangapi wanatoka Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa maelezo yake mazuri na vijana wetu wanasikia kwamba vipi uteuzi huo unavyoelekea. Baada ya maelezo hayo ningeomba kujua, makubaliano yao yanakuwa baina ya SMT na SMZ na wanateua hao vijana. Je, huduma za vijana hao kutoka Zanzibar hadi kufika chuoni huwa zinafadhiliwa na nani SMT au SMZ? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; vijana ambao tayari huwa wanawateua percentage kubwa ni wanaume kuliko wanawake na wanawake kwa kipindi hiki wanachacharika katika kupata elimu. Je, mtazamo huo unakuwa uko namna gani hata vijana wanawake wanakuwa kidogo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Fakharia, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi; ufadhili kwa wanafunzi hawa wanaokwenda nje unafadhiliwa na nchi zile ambazo wanafunzi hawa wanakwenda na siyo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wala siyo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa hiyo taratibu zote zile za kugharamia yale masomo huwa zinafanywa na zile nchi husika; ingawa sasa hivi sisi kama Serikali tumetoa fursa kwa Bodi yetu ya Mikopo kuweza kuwa na ile partial scholarship. Kuna baadhi ya wanafunzi ambao wanafadhiliwa kupitia Bodi zetu ile Zanzibar pamoja na hii ya Tanzania Bara kwa kupata partial scholarship; kwa hiyo utaratibu wake unakuwa hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili amezungumza habari ya wanaume kuwa wengi kuliko wanawake. Kwanza tukiri kwa sababu takwimu zinaonesha hapa wanaume ni asilimia 71 na wanawake ni asilimia hiyo 29. Hii inatokana na zile sifa kwa sababu hawa wanapochaguliwa kwenda kufanya masomo kwenye nchi hizi za nje kuna sifa ambazo zinaorodheshwa pale pamoja na ufaulu. Kwa hiyo, hii nadhani inatokana na ile namna gani wanaume wanafaulu kuliko wanawake.

Mheshimwa Naibu Spika, kwa vile Mheshimiwa Mbunge amelileta jambo hili hapa, basi sasa labda katika ugawaji hata zile nchi tutaziambia angalau ziweze kufanya fifty fifty ili na wanawake wengi waweze kupata fursa hii. Nakushukuru sana.

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, ni vijana wangapi wamepata nafasi za masomo nje ya nchi kwa mwaka 2015 - 2020 na kati yao ni wangapi wanatoka Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Nataka kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri mwelekeo wa Serikali kutafuta scholarship ni katika maeneo gani hususan ambayo inataka wanafunzi wetu waende kusoma. Vilevile ukiangalia idadi ya wanafunzi 400 kwa Taifa hili ni kidogo sana ambao wamepata scholarship. Je, mpango wa Serikali ni upi hasa wenyewe makusudi kutafuta scholarship nje ya nchi ili iweze kuongeza idadi ya Watanzania wengi waweze kwenda kusoma nje ya nchi? Ahsante sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, ingawa amezungumzia maeneo mawili ambayo kipaumbele ni vipi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba nchi hizi zinapotoa ufadhili kwenye hizi scholarship ni nchi zenyewe ndizo ambazo zina-detect, zinazoamua kwamba kozi gani ziende zikasomewe; lakini maeneo mengi sana yamekuwa ni maeneo ya Udaktari pamoja na Uhandisi. Pia naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mwaka ujao wa fedha, sisi kama Serikali kwanza tumeviagiza vyuo vyetu vikuu viweze kuandaa au kupendekeza maeneo ambayo wanafunzi wa Kitanzania watakwenda kufanya masomo yao nje ya nchi.

Mheshimwa Naibu Spika, vile vile kama nilivyoeleza katika swali la nyongeza ni kwamba, Serikali kupitia Bodi ya Mikopo tumekuwa tukifadhili baadhi ya scholarship kwa kupata partial mikopo kwa ajili ya vijana wetu ambao wanakwenda kusoma nje. Kwa hiyo, huo ndiyo mkakati wetu kama Serikali na tutaendelea kufanya hivyo wakati upatikanaji wa fedha utakapokuwa mzuri. Nakushukuru sana.