Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE (K.n.y MHE. ROSE K. SUKUM) aliuliza:- Serikali ina utaratibu wa kutoa fedha kwa ajili ya shule za bweni nchini. Kwa kipindi cha kuanzia tarehe 31/08/2013 hadi tarehe10/02/2014 Halmashauri ya Hanang ilipokea kutoka Serikali Kuu kiasi cha shilingi 508,779,500 kwa ajili ya chakula cha shule za bweni. Taarifa zinaonesha kwa fedha zilizotumika kununua chakula ni shilingi 225,585,000 kwa takwimu hizo bakaa ni shilingi 283,194,500 kwa mujibu wa Mkaguzi, bakaa hiyo haionekani kwenye account yoyote benki. (a) Je, fedha hizo zinarudishwa Hazina bila ya kuwa na uwepo wa nyaraka zozote toka Halmashauri kuonesha muamala unavyofanya kazi? (b) Je, kama fedha hizo hazikurudishwa Hazina nani anaweza kuidhinisha matumizi bila ya mpango wake kupitishwa na Kamati ya Fedha na Mipango ya Halmashauri? (c) Je, kama fedha zimetumika bila kupangiwa na Kamati halali, ni kwa nini wahusika bado wanaendelea kuwa ofisini bila ya kufunguliwa mashtaka ya wizi wa kuaminika?

Supplementary Question 1

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niipongeze Serikali kwa kupeleka fedha hizi kwenye shule za bweni zilizoko kwenye Wilaya ya Hanang. Pamoja na hatua hiyo nzuri na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nilikuwa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa kushirikiana na Mbunge wao wamefanya kazi kubwa sana ya kujenga shule pamoja na hosteli kwenye shule za Isaka, Baloha, Mwalimu Nyerere, Lunguya pamoja na Busangi. Lakini shule hizi au hosteli hizi hazitambuliki kabisa na Serikali kwa maana ya kutolewa au kupewa msaada wa aina yoyote kama inavyofanyika kwa wenzao wa Hanang. Je, Serikali inaweza sasa ikaziingiza shule hizi kwenye mpango wa kupatiwa huduma ya chakula kama ilivyofanyika kwenye maeneo mengine nchini?
Swali la pili, kwa kuwa tatizo la mabweni kwenye shule nyingi za sekondari za kata ni kubwa sana hasa kwenye shule zilizoko kwenye maeneo ya wafugaji ambao wengi wao wanaishi kwenye maeneo ya pembezoni na yenye mazingira magumu, na kwa kutambua mazingira hayo wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa kushirikiana na Mbunge wao wameanza juhudi au wanaendelea na juhudi za kujenga hosteli kwenye shule ambazo bado hazijapata ikiwemo shule za sekondari za Isakajana, shule za sekondari za Ngaya pamoja na zingine.
Je, Serikali inaweza ikachangia namna gani au ikaunga mkono namna gani juhudi hizi nzuri za wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala pamoja na Mbunge wa eneo hilo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mbunge huyu pamoja na wananchi wake kuhakikisha kwamba wamejenga hosteli katika shule hizo za kata, lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba vijana especially wa kike au wanafunzi wa kike waweze kusoma katika mazingira rafiki. Mheshimiwa Maige nakumbuka kwamba tulikuwa pamoja katika gari yangu tukisafiri kutoka Msalala pale Mjini tukaenda mpaka kule Bulyanhulu, kwa hiyo ninalijua vizuri jiografia ya eneo lako. Naomba nikupongeze katika harakati kubwa ulizofanya na wenzako wa kule Msalala.
Mheshimiwa Naibu Spika, ombi lako katika eneo la kwanza ulikuwa unaomba kwamba ikiwezekana shule hizi sasa ziingizwe katika utaratibu mwingine wa Kiserikali sasa vijana wa maeneo haya waweze kupewa chakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mchakato wetu mpana tulioufanya na hili nimezungumza katika vipindi tofauti kwamba lengo kubwa lilikuwa kwanza programu ya kwanza ni ujenzi wa shule za kata, lakini suala lingine la pili inaonekana kwamba vijana wengi wanaoenda shule za kata wanapata ushawishi mkubwa sana kurubuniwa katikati tumejikuta kwamba vijana wengi wanapata ujauzito.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeelekeza maeneo mbalimbali kwamba zile shule za Kata zilizojengwa angalau ikiwezekana wazazi waone kama kutakuwa na utaratibu wa ujenzi wa mabweni ili kuweza kuwa- accomodate vijana katika mazingira ya karibu zaidi na shule. Jambo hili naomba nishukuru karibu Tanzania nzima limefanyika kwa upana mkubwa zaidi, lakini kuna shule maalum za bweni ambazo zinatambuliwa na Serikali, lakini kuna zile zingine hosteli zimejengwa na wananchi wenyewe. Tunachokifanya sasa hivi Serikali ni kumebainisha zile shule ambazo ziko katika mkakati wa Kiserikali kama tunavyozijua zile shule za Kitaifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hivi sasa siwezi kuzungumza wazi kwamba kusema kwamba shule zote ambazo mabweni yamejengwa kwamba zitapewa chakula jambo hilo litakuwa ni jambo la uongo. Isipokuwa Serikali tunaangalia jambo hili kwa uzito wake na kufanya tathmini ya kina basi hapo baadaye kama tulivyoenda na programu ya elimu bure katika analysis ya kutosha hapo baadaye kuzibainisha baadhi ya shule tuzi - upgrade ziwe special shule za hosteli jambo hili Serikali hatutosita kuliangalia lakini jambo kubwa hilo tutafanya analysis kwa nchi nzima tutafanyaje kazi kuhakikisha mazingira bora yanatengenezwa kwa vijana wetu wasichana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika sehemu ya pili ni kwamba kuna baadhi shule zingine bado hazijapata hosteli, naomba nikuunge mkono tena kwamba endelea na juhudi ile ile. Lakini naomba nikuahidi kwamba katika mipango yenu ya Halmashauri ikiwezekana ninavyofanya mchakato wa bajeti za Halmashauri wekeni vipaumbele hivyo na Ofisi ya Rais, TAMISEMI nia yake itakuwa ni kuweza kusukuma juhudi hizi za wananchi ifike muda kwamba shule zote ambazo zina changamoto kubwa tuweze kusaidia zipate mabweni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali lengo kubwa ni kwamba vijana wetu hasa wasichana watakuwa wanakwepa hivi vishawishi ambavyo vimekuwa ni tatizo kubwa sana na likiwagharimu vijana wengi kupata ujauzito.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE (K.n.y MHE. ROSE K. SUKUM) aliuliza:- Serikali ina utaratibu wa kutoa fedha kwa ajili ya shule za bweni nchini. Kwa kipindi cha kuanzia tarehe 31/08/2013 hadi tarehe10/02/2014 Halmashauri ya Hanang ilipokea kutoka Serikali Kuu kiasi cha shilingi 508,779,500 kwa ajili ya chakula cha shule za bweni. Taarifa zinaonesha kwa fedha zilizotumika kununua chakula ni shilingi 225,585,000 kwa takwimu hizo bakaa ni shilingi 283,194,500 kwa mujibu wa Mkaguzi, bakaa hiyo haionekani kwenye account yoyote benki. (a) Je, fedha hizo zinarudishwa Hazina bila ya kuwa na uwepo wa nyaraka zozote toka Halmashauri kuonesha muamala unavyofanya kazi? (b) Je, kama fedha hizo hazikurudishwa Hazina nani anaweza kuidhinisha matumizi bila ya mpango wake kupitishwa na Kamati ya Fedha na Mipango ya Halmashauri? (c) Je, kama fedha zimetumika bila kupangiwa na Kamati halali, ni kwa nini wahusika bado wanaendelea kuwa ofisini bila ya kufunguliwa mashtaka ya wizi wa kuaminika?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, shule hizi za bweni zimekuwa zikipelekewa fedha shilingi 1,500 kwa siku kwa mwanafunzi. Je, nilitaka kujua ni lini Serikali itaongeza hizi fedha ili shule zetu za bweni zisifungwe mapema na kuchelewa kufunguliwa ili watoto wapate muda mwingi wa kusoma wakiwa shuleni? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, anachozungumzia ni unit cost ya chakula kwa mwanafunzi, na concern hii nadhani Wabunge wengi walikuwa wameelezea kusema na hii rate ya shilingi 1,500 ni ndogo. Unit cost siyo kwa ajili ya chakula peke yake isipokuwa kwa ajili ya mchakato mzima wa elimu, jambo hili watalamu wetu sasa hivi wanalifanyia kazi pale litakapokamilika tutaangalia ni jinsi gani kama kuna uwezekano kupandisha gharama hii kidogo ili mtoto apate lishe ya kutosha ya kuweza kumfanikisha aweze kupata masomo vizuri. Kwa sababu tunajua kwamba suala la lishe ni jambo la msingi sana kujenga akili ya mtoto.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ni kwamba jambo hili tunalifanyia kazi sasa hivi kuangalia unit cost kwa shilingi 1,500 ni kweli tutafanyaje sasa na iende mpaka kiasi gani kwa kuangalia uwezo wa Serikali kwa muda muafaka.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE (K.n.y MHE. ROSE K. SUKUM) aliuliza:- Serikali ina utaratibu wa kutoa fedha kwa ajili ya shule za bweni nchini. Kwa kipindi cha kuanzia tarehe 31/08/2013 hadi tarehe10/02/2014 Halmashauri ya Hanang ilipokea kutoka Serikali Kuu kiasi cha shilingi 508,779,500 kwa ajili ya chakula cha shule za bweni. Taarifa zinaonesha kwa fedha zilizotumika kununua chakula ni shilingi 225,585,000 kwa takwimu hizo bakaa ni shilingi 283,194,500 kwa mujibu wa Mkaguzi, bakaa hiyo haionekani kwenye account yoyote benki. (a) Je, fedha hizo zinarudishwa Hazina bila ya kuwa na uwepo wa nyaraka zozote toka Halmashauri kuonesha muamala unavyofanya kazi? (b) Je, kama fedha hizo hazikurudishwa Hazina nani anaweza kuidhinisha matumizi bila ya mpango wake kupitishwa na Kamati ya Fedha na Mipango ya Halmashauri? (c) Je, kama fedha zimetumika bila kupangiwa na Kamati halali, ni kwa nini wahusika bado wanaendelea kuwa ofisini bila ya kufunguliwa mashtaka ya wizi wa kuaminika?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi hii.
Kwa kuwa, Wilaya ya Hanang ni Wilaya ya wafugaji, na wananchi wamejitahidi sana kujenga hosteli kama ya shule ya Mreru, Mulbadau, Endasak na kwa kufuatia suala hilo; je, Serikali ipo tayari kusaidiana na wananchi, kuona kwamba zile hosteli na mabweni yaliyokuwepo toka wakati wa uhuru, tunaimarisha na kuboresha miundombinu ambayo ipo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge senior katika Bunge hili amesema jinsi gani Serikali itaboresha hizi shule, ni kweli shule ambazo zimejengwa muda mrefu lazima tuangalie ni jinsi gani tutaboresha miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nilikuwa katika Chuo cha Kigurunyembe, nimepitia shule mbalimbali. Kuna baadhi ya shule zamani zilikuwa zinafanya vizuri zaidi, lakini kutokana na uchakavu wa miundombinu ufanisi wake umekuwa chini sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilipotembelea shule ya Iyunga kule Mbeya ambayo bweni lake liliungua, nilivyoangalia nikaona ni kwa nini sasa shule nyingi ambazo zamani zilikuwa ni shule za vipaji lakini sasa hivi uwezo wake umekuwa chini, bunsen banner iliyokuwa inatumika mwaka 1980, ndiyo inayotumika mpaka mwaka 2017; jambo hili haliwezekani.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie kwamba, jukumu letu kubwa ikiwezekana katika Halmashauri tubainishe katika vipaumbele kwa sababu tumekuwa na tatizo kubwa sana la kufanya ukarabati katika shule zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuungane kwa pamoja, tubainishe shule zilizochakaa katika mipango yetu ya Halmashauri katika bajeti tuliweke hili mapema, Ofisi ya Rais TAMISEMI itaweka nguvu kuhakikisha kwamba shule hizi sasa zinakuwa na ubora ili wanafunzi waweze kupata taaluma inayokusudiwa na shule zetu za Serikali ziwe shindani sawa na shule nyingine za private katika Jamhuri wa Muungano wa Tanzania..

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE (K.n.y MHE. ROSE K. SUKUM) aliuliza:- Serikali ina utaratibu wa kutoa fedha kwa ajili ya shule za bweni nchini. Kwa kipindi cha kuanzia tarehe 31/08/2013 hadi tarehe10/02/2014 Halmashauri ya Hanang ilipokea kutoka Serikali Kuu kiasi cha shilingi 508,779,500 kwa ajili ya chakula cha shule za bweni. Taarifa zinaonesha kwa fedha zilizotumika kununua chakula ni shilingi 225,585,000 kwa takwimu hizo bakaa ni shilingi 283,194,500 kwa mujibu wa Mkaguzi, bakaa hiyo haionekani kwenye account yoyote benki. (a) Je, fedha hizo zinarudishwa Hazina bila ya kuwa na uwepo wa nyaraka zozote toka Halmashauri kuonesha muamala unavyofanya kazi? (b) Je, kama fedha hizo hazikurudishwa Hazina nani anaweza kuidhinisha matumizi bila ya mpango wake kupitishwa na Kamati ya Fedha na Mipango ya Halmashauri? (c) Je, kama fedha zimetumika bila kupangiwa na Kamati halali, ni kwa nini wahusika bado wanaendelea kuwa ofisini bila ya kufunguliwa mashtaka ya wizi wa kuaminika?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Nashukuru Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuniona, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, na mimi naomba kuuliza swali dogo la nyongeza, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini.
Katika Jimbo la Mafinga Mjini tuna shule mbili za sekondari za bweni, mojawapo ni shule ya sekondari ya bweni ya Changarawe. Katika kutekeleza majukumu kama wananchi, bodi ya shule kwa kushirikiana na wazazi imeanza na inaendeleza jitihada za kujenga jiko la kudumu na bwalo la chakula kwa ajili ya wanafunzi hao. (Makofi)
Je, Serikali kwa kilio changu kile kwamba hii ni Halmashauri mpya ipo tayari kwa kutuongezea nguvu ili kukamilisha jiko hilo la kudumu na bwalo la chakula kwa ajili ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Changarawe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anasema ujenzi wa bweni pamoja na jiko katika Shule ya Sekondari ya Changarawe, naomba niseme kwamba nimelisikia hili jambo, Mheshimiwa Cosato Chumi tumezungumza mambo mengi, ukiachia miradi yake ya maji iliyokuwa imekwama amepambana, na hili naomba niseme kwa sababu hapa siwezi kusema kuna bajeti special kwa ajili ya bweni hili, lakini katika mchakato wetu, kama tulivyoahidiana kwamba mara baada ya Bunge tutapitia, nitakwenda kukagua Shule ya Sekondari ya Iyunga ambayo ujenzi wa mabweni unaendelea, tutapita kuangalia kwa pamoja, mikakati gani tuifanye ili bweni likikamilika na jiko likikamilika, watoto watakula na kuishi sehemu rafiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hatuoni tatizo katika eneo hilo, lakini ni lazima tushirikishane kwa pamoja tuangalie ni mkakati gani wa haraka utaweza kusaidia katika eneo hili la Shule ya Sekondari ya Changarawe. Mheshimiwa Mbunge, naomba niseme kwamba jambo hili nimelipokea tutakapokuwa pale field tutapanga mikakati ya pamoja lengo ni kuwasaidia vijana wetu.