Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasilisha Muswada wa Sheria unaozuia Polisi kukamata na kuwashikilia watuhumiwa kabla ya kukamilisha upelelezi?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru nina swali moja dogo la nyongeza.

Kwa kuwa, idadi kubwa ya mahabusu walioko kwenye magereza zetu wanaipa mzigo mkubwa sana Serikali yetu kuwahudumia. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuleta sheria ambayo itawezesha watuhumiwa wakapewa nafasi ya kujidhamini wenyewe ili kuipunguzia Serikali mzigo na kuwapunguzia adha wananchi wanaotekesaka kwenye magereza, kwa makosa mbalimbali ambayo kimsingi yanaweza kudhaminika?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la mtuhumiwa kujidhamini au kudhaminiwa ni kuhakikisha kwamba anarudi mahakamani kwa tarehe itakayotakiwa. Kwa hivi sasa Serikali imejikita katika mpango wa kuweka anwani za makazi pindi zoezi hili litakapokamilika tutakuwa na uwezo wa kujua kila mtu anaishi wapi, hivyo kutakuwa na uwezekano wa kujidhamini wenyewe. Kwa hiyo, kazi ambayo Mheshimiwa Nape anaifanya ikikamilika, pamoja na vitambulisho vya Taifa NIDA, itawawezesha Watanzania kujidhamini wenyewe, hivyo kupunguza msongamano wa mahabusu ambao watakuwa wako nje. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasilisha Muswada wa Sheria unaozuia Polisi kukamata na kuwashikilia watuhumiwa kabla ya kukamilisha upelelezi?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa kero kubwa ya msongamano wa mahabusu na wafungwa magerezani imekithiri. Je, Serikali inaonaje ikaleta utaratibu wa vifungo vya nje kwa makosa madogo madogo ili kupunguza msongamano huo? Ahsante.

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunapitisha bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria mwaka huu, tulisema moja kati ya vipaumbele ni kwenda kuangalia upya, kuufumua na kuupanga upya mfumo wa jinai hapa nchini. Katika mpango huo moja kati ya jambo ni hili kuangalia adhabu mbadala ambazo zitasaidia kupunguza msongamano wa mahabusu magerezani. (Makofi)