Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka shilingi milioni 500 ya ujenzi wa Kituo cha Afya Namiungo na shilingi milioni 200 ya Kituo cha Afya cha Nakayaya?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Kituo cha Afya cha Namiungo, ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ambaye ni Hayati, alitoa ahadi Milioni 500 ili kuweze kukamilisha Kituo cha Afya cha Namiungo. Sasa je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Kituo cha Afya cha Nakapanya, kilitengewa fedha kiasi cha shilingi milioni 400 mwaka wa fedha 2021 na kilipokea shilingi milioni 200 na kujenga majengo ya upasuaji pamoja na maabara.
Je, ni lini Serikali itatupatia kiasi kilichobaki ili kuweza kujenga majengo mengine muhimu kama vile mortuary na mionzi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeza sana Mheshimiwa Kungu kwa namna ambavyo anawakilisha kwa dhati wananchi wa Tunduru Kaskazini, na nimhakikishie kwamba ahadi ya Mheshimiwa Rais ni kipaumbele cha Serikali. Tunafahmu kwamba Namiungo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, nasi tayari tumeshaweka mpango wa kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Namiungo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na Kituo cha Afya cha Nakapanya, hiki ni kituo kati ya vituo 52 ambavyo katika mwaka wa fedha huu tumetenga Bilioni 15.6 kwa ajili ya umaliziaji wa vituo hivi kikiwemo kituo hiki cha afya cha Nakapanya. Ahsante.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka shilingi milioni 500 ya ujenzi wa Kituo cha Afya Namiungo na shilingi milioni 200 ya Kituo cha Afya cha Nakayaya?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Je, ni lini Serikali itapeleka Shilingi Milioni 200 katika Kituo cha Afya cha Nyalioba, ikiwa ni ni utekelezaji wa ahadi ya Makamu wa Rais, Dkt. Philip Isdor Mpango?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Florence Samizi, Mbunge wa Jimbo la Muhambwe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza sana Mheshimiwa Dkt. Samizi anawasemea sana wananchi wa Jimbo la Muhambwe, nakumbuka katika ziara ya Mheshimiwa Makamu wa Rais tulikuwa pamoja tuliahidi Milioni 200 Mheshimiwa Makamu wa Rais aliahidi. Ninakuhakikishia kwamba Ofisi ya Rais – TAMISEMI tayari imetenga fedha hizo na wakati wowote zitaingia kwenye Kituo cha Afya cha Nyalioba, ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka shilingi milioni 500 ya ujenzi wa Kituo cha Afya Namiungo na shilingi milioni 200 ya Kituo cha Afya cha Nakayaya?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Mheshimiwa Hayati Dkt. Magufuli mwaka 2018 aliahidi kutoa Shilingi Milioni 100 kumalizia Kituo cha Afya cha Mchomoro, lakini mpaka leo fedha hizo hazijapatikana. Je, Serikali iko tayari kuzitoa fedha hizo ili kuendeleza Kituo cha Afya cha Mchomoro?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza sana Mheshimiwa Kawawa kwa kazi kubwa anayofanya kuwasemea wananchi wa Namtumbo, na nimhakikishie kwamba ahadi ya Mheshimiwa Rais ni kipaumbele, tunafahamu milioni 100 inahitajika katika kituo hiki cha Namchomoro na tutaleta fedha hiyo kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho. Ahsante.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka shilingi milioni 500 ya ujenzi wa Kituo cha Afya Namiungo na shilingi milioni 200 ya Kituo cha Afya cha Nakayaya?

Supplementary Question 4

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mwaka jana Wabunge wote tulitoa vipaumbele vya vituo vya afya kwenye Kata mbalimbali nchini. Je, ni lini Serikali itatupatia fedha za Kituo cha Afya cha Kata ya Ruvu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mwakamo, amekuwa mchapakazi sana, mwakilishi mzuri wa wananchi wa Jimbo la Kibaha Vijijini, tunafahamu kwamba Kata ya Ruvu inahitaji kituo cha afya, kwa sasabu ya idadi ya wananchi waliopo na tayari tumeweka kwenye mpango mkakati kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Ruvu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante. (Makofi)