Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatunga Sheria ya Uanzishwaji wa Baraza la Taaluma kwa Kada ya Ustawi wa Jamii?

Supplementary Question 1

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini sambamba na hilo nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; naomba kupata commitment ya Serikali kuhusiana na kutunga sheria hii. Je, sheria hii itaweza kutungwa ndani ya uhai wa Bunge hili?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa, sheria imechukua muda mrefu kutungwa. Je, Serikali haioni sababu ya kutengeneza mkakati au mpango maalum wa kuona jinsi ya kuweza kuwaangalia hawa Maafisa Ustawi ambao wanakiuka taratibu? Ahsante.

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Toufiq, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, inaona umuhimu wa sheria hii. Kama nilivyoeleza katika jibu langu la msingi Serikali itasimamia sheria hii ili iweze kuwasilishwa mapema katika Bunge hili Tukufu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili kuhusu Maafisa Ustawi kuwa na maadili. Ushauri umepokelewa. Hata hivyo, Wizara inafuata kanuni za utumishi wa umma kwa wafanyakazi wote na wafanyakazi wote wanaokiuka maadili, hatua za kisheria zinachukuliwa pale wanapofanya makosa. (Makofi)