Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa bei elekezi ya vifaa vya tiba hasa vya macho, pua na koo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; ninapozungumzia tiba ya macho, pua na koo, nazungumzia ongezeko la mabubu na viziwi nchini. Sasa kwa kuwa, kumekuwa na ongezeko kubwa la mabubu na viziwi nchini ambalo limesababisha Serikali kupeleka ruzuku kwa wanafunzi kutoka bilioni 3.6 mwaka 2018/2019 mpaka bilioni 6.3 mwaka 2021/2022. Je, Serikali haioni haja ya kupeleka vifaa vya kupima usikivu kwenye hospitali za wilaya ili kila mtoto anapozaliwa aweze kupimwa usikivu ili kupunguza tatizo la ububu na uziwi nchini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa, tangu mwaka 2016/2017, Serikali ilianzisha upasuaji wa kupandikiza vifaa vya usikivu nchini. Je, ni juhudi gani zimefanyika kuongeza vitengo vya speech therapy katika hospitali zetu, ili kuondosha tatizo la mabubu na viziwi nchini? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja anaulizia ni kwa namna gani Serikali itajipanga kupeleka vifaa tiba kwenye level ya wilaya. Tunapokea ushauri wake na sio tu kwenye eneo la kupeleka vifaa kwa ajili ya kupima watu wenye matatizo hayo, lakini ni ku-include kwenye package ya mama anayejifungua, wakati anajifungua basi mtoto aweze kuhakikishwa kwamba amechunguzwa vitu vyote kiasi kwamba, hata wakati anahudhuria clinic kuna uchunguzi kama huo ili kuwatambua mapema na kuwasaidia.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kwamba, toka 2016 kulikuwa na operation za kuweka vipandikizi kwa wale watu ambao wana shida ya usikivu; tunapokea ushauri wake na bado tunasema hivyohivyo kama kwenye issue ya suala zima la watoto wadogo, vilevile tutapeleka kwa kuanzia kwenye level za mikoa kuhakikisha operations kama hizo zinaweza kufanyika na watu wao kupata huduma, lakini vilevile kwa watu ambao tayari wana tatizo hilo tunatengeneza utaratibu wa kuwasaidia hasa wanapokuja hospitali, watu wanaoweza kufafanua zile lugha za ishara na mambo mengine, ili waweze kupata huduma kama watu wengine. Ahsante sana.

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa bei elekezi ya vifaa vya tiba hasa vya macho, pua na koo?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kituo cha Afya cha Kambarage kilichopo Manispaa ya Shinyanga Mjini ambacho ni tegemeo kubwa sana kwa wananchi na hasa akinamama kwa kuwa kinazalisha akinamama takribani 330 kwa mwezi, kinakabiliwa na tatizo kubwa sana la ukosefu wa generator. Kiasi cha shilingi milioni 290 ambayo ilitolewa katika mpango wa Serikali kuboresha vituo vya afya ilitolewa na ikakabidhiwa MSD, vifaa tiba vingi vimekuja kasoro generator, wananchi wanalalamika. Je, ni lini generator litakuja kama sehemu ya vifaa-tiba katika Kituo hicho cha Afya cha Kambarage? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nimetembelea hicho kituo na nimekuta Mheshimiwa Mbunge alichangia milioni 18 kwa ajili ya ujenzi wa hicho kituo, lakini ninachoweza kusema ni tukishamaliza maswali hapa, tukutane mimi na yeye, tutashirikiana na mwenzangu wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ili tuweze kuhakikisha kwamba, vifaa hivyo vinafika kwa sababu, kama fedha zimepelekwa, basi ni kupeleka kile ambacho kinatakiwa kufanyika. Tukae mimi na yeye tuhakikishe generator limeenda.