Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza miundombinu ya Vyuo Vikuu nchini kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, pamoja na jitihada za Serikali kuongeza miundombinu zinazoendelea, bado kuna baadhi ya kozi hazitolewi hapa nchini.

Je, Serikali haioni haja ya kushirikiana na vyuo vingine nchi za nje ili kutoa kozi hizo hasa katika sekta ya afya.

Swali la pili, pamoja na mkakati huu wa miundombinu, Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Wahadhiri katika Vyuo Vikuu hapa nchini? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Pauline Nahato kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la kwanza, kwanza tukiri kwamba kuna baadhi ya kozi katika Sekta ya Afya ni kweli hazitolewi hapa nchini. Lakini nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, katika kipindi kifupi tumeweza kupata uzoefu kutokana na janga hili la UVIKO-19 kuna wanafunzi wengi sana walirejeshwa hapa nchini, vilevile kama mnavyofahamu mwezi Februari, Machi mwaka huu kutokana na vita vya Ukraine pamoja na Urusi wanafunzi wengi wameweza kurejeshwa miongoni mwao ni wale ambao walikuwa wanachukua kozi ya ambazo hazipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeanza mjadala wa kuangalia namna gani tunaweza kuangalia mashirikiano ya karibu ya kuangalia tunaweza kushirikiana vipi na vyuo vingine vya nje ya nchi ili kozi hizo zinaweza zikatolewa kule kwa ushirikiano vilevile na hapa nchini. Naomba tulibebe wazo hili lakini tubebe ushauri huu wa Mheshimiwa Paulina tuendelee kuufanyia kazi kuweza kuangalia kozi hizi ambazo hazitolewi namna gani tunaweza tukazifanya kwa mashirikiano na vyuo vingine vya nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa eneo la pili la uongezaji wa Wahadhiri, nadhani swali hili nimeshawahi kulijibu hapa Bungeni. Kwanza kupitia mradi wa HEET tunakwenda kusomesha Wahadhiri wapya zaidi ya 1,000. Kwa hiyo, pamoja na uongezaji huu wa miundombinu lakini utakwenda sambamba na kusomesha Wahadhiri katika awamu ya kwanza karibu Wahadhiri 625 tunakwenda kuwasomesha wa kozi ndefu lakini wale kozi fupi zaidi ya Wahadhiri 400. Kwa hiyo, tunaamini tunaweza kupunguza uhitaji huo wa Wahadhiri kwenye vyuo vyetu.

Mheshimiwa Spika, eneo la pili Serikali mara nyingi sana huwa inatoa vibali vya kuajiri walimu wapya, wahadhiri wapya nao vilevile mfumo huo tutautumia. Lakini vyuoni kule kuna mpango vilevile vyuo vyenyewe huwa vinakuwa na mpango wa kusomesha Wahadhiri na kuajiri wale Wahadhiri wa mikataba ya muda mfupi. Kwa hiyo, mipango hii yote tukiijumuisha tunakwenda kuondoa tatizo hili la Wahadhiri.

Mheshimiwa Spika, kama mnavyofahamu Serikali yetu imeweza kuongeza mikopo ile ya elimu ya juu kwa wanafunzi wale ambao wanaoingia katika elimu ya juu, eneo hili kwa vile tutakuwa na udahili mkubwa wa wanafunzi wa elimu ya juu, ni dhahiri kabisa tutaweza kupata wahadhiri wa kutosha kwenye vyuo vyetu hivi ambavyo tunatarajia kuvijenga. Nakushukuru sana.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza miundombinu ya Vyuo Vikuu nchini kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa Mikoa mikubwa sana hapa nchini na wenye wanafunzi wengi. Je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa Kampasi ya Chuo Kikuu katika Mkoa wa Kagera?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza Mheshimiwa Dkt. Kikoyo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, wakati najibu swali la msingi nimezungumza mradi wetu wa HEET, kwamba pamoja na mambo mengine unakwenda vilevile kujenga vyuo katika Mikoa ya pembezoni na miongoni mwa Mikoa ambayo niliitaja ni pamoja na Mkoa wa Kagera. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nadhani Mkoa huu upo na upo kwenye program hii HEET tutakwenda kujenga chuo katika Mkoa huo wa Kagera pamoja na Mikoa mingine ya pembezoni. Nakushukuru sana.

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza miundombinu ya Vyuo Vikuu nchini kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID ABDALLA RASHID: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi Zanzibar imeshatoa eneo kwa ujenzi wa Chuo Kikuu Huria na Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere katika eneo la Mfikiwa. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Rashid Rashid kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyowaeleza kwenye majibu ya msingi, mradi wetu wa HEET unakwenda ku-cover karibu maeneo mengine sana. Amezungumza hapa suala la Chuo Kikuu Huria pamoja na Chuo chetu cha Mwalimu Nyerere ambayo tayari ina Kampasi kule Zanzibar, kwa hiyo, ni suala tu la upanuzi Kwa vile amezungumza hapa kwamba kuna eneo ambalo tayari limeshatolewa tunaomba tuchukue wazo hili tuweze kuangalia namna gani ile Kampasi iliyopo pale Zanzibar inaweza kupanuliwa kwa ajili ya kwenda eneo hilo ambalo Mheshimiwa Mbunge amelitaja. Nakushukuru sana.