Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kuhamasisha kilimo cha zao la Mwani?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Swali langu la nyongeza ni kwamba nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Je, Pamoja na juhudi nzuri walizofanya kuhakikisha zao la mwani linakuzwa.

Je, Serikali imefanya juhudi gani kuhakikisha wakulima hawa wanapata soko ambalo litakidhi haja ya kilimo chao?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Said Issa Mbunge wa Konde kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya jitihada ya kutafuta masoko na kwa sasa tuna masoko katika nchi za Marekani, Ufaransa na Spain. Kwa umuhimu zaidi tumeanza mazungumzo na Shirika la Usafirishaji, Tumeanza mazungumzo na shirika la usafirishaji la DHL ili kuweza kuhakikisha kwamba wazalishaji kwa maana ya wakulima wanapata masoko Kimataifa moja kwa moja kwa kuwa tumeshapata kujua juu ya nini soko linahitaji, mawasiliano ya moja kwa moja.

Mheshimiwa Spika, hatua ya pili tunashukuru katika bajeti ya mwaka huu tunaouendea 2022/2023 Serikali imetenga fedha za kutosha za kuhakikisha wakulima wanaongeza thamani ya zao hili. Kwa hivyo, tutakuwa na mashine za ukaushaji wa Mwani katika mwambao wote wa Pwani, kuanzia Tanga, Pwani mpaka Lindi na Mtwara kwa lengo la kuhakikisha tunaongeza thamani ya zao letu la Mwani ili tuweze kulingana na mahitaji ya soko. Ahsante sana.

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kuhamasisha kilimo cha zao la Mwani?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na mimi kunipatia fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Kwa vile zao hili la Mwani zaidi ya asilimia 80 ndiyo tunategemea mauzo ya nje, lakini zaidi ya asilimia 20 ndiyo inabakia kwa ajili ya kulichakata na kutengeneza bidhaa mbalimbali ambazo zinabaki ndani ya nchi. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutoa elimu hasa kwa wale wakulima wetu ndani ya nchi kuweze kutengeneza bidhaa ambazo zitakuwa na soko pia zitakuwa na quality pia zitakuwa zinauzika ndani ya nchi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamad kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, juu ya mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba tunaongeza thamani kama nilivyokwisha kueleza kwenye jibu la msingi. Kwanza Mwani wetu mwingi unakaushwa katika michanga, Mheshimiwa Hamad na Wabunge wa kutoka katika Mikoa hii ya huku Pwani inayolima Mwani wanaweza kuwa ni mashahidi wangu. Ndiyo maana tumejielekeza katika kuhakikisha kwamba tunapata kitu kilicho na ubora kwa kwenda kupeleka mashine za kukausha huu Mwani ili kusudi twende katika hatua inayofuata sasa ya kuongeza thamani kutengeneza sabuni, shampoos, bidhaa za chakula kwa ajili ya kuongeza hii thamani. Kama haitoshi, mbele zaidi tunataka tuanze kufanya extraction.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri ngoja ngoja kwa sababu muda wa kujibu swali ni mfupi, anataka kujua mpango wa elimu kwa hao wakulima wa Mwani.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, shukrani sana. Kama nilivyoeleza katika jibu la msingi elimu tayari ilishatolewa na tunaendelea kutoa. Kwa hivyo, tutaendelea na mpango wa utoaji wa elimu katika vikundi vyote tunawaunganisha wakulima wa Mwani ili kuweza kuwa rahisi kwa kazi yetu ya utoaji wa elimu katika Mwambao mzima wa Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi. Ahsante.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kuhamasisha kilimo cha zao la Mwani?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa vile wanaojishughulisha sana na zao la Mwani ni wanawake. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapa wanawake hao nyenzo za kisasa kwa ajili ya kilimo hicho?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tulishakwisha kuanza kutoa zana kama vile Kamba na ipo zana inaitwa taitai na hilo zoezi tutaendelea nalo ikiwa ni pamoja na matarajio yetu ya kununua boti ambazo zitakwenda kwa ajili ya wavuvi lakini na vikundi vya akina mama kwa ajili ya wakulima wa Mwani kuweza kuyafikia maeneo yale pale maji yanapokuwa mengi na uvunaji wa ule Mwani. Ahsante sana.