Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya mawasiliano katika Kata za Idete, Kiyowela, Maduma, Idunda, Makungu na Ihowanza?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Niishukuru kwanza Wizara kwa kazi kubwa sana ambayo wameifanya, wamekwishaanza. Maswali yangu mawili ya nyongeza ni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza; kwenye Kata ya Kasanga ndiyo Makao Makuu ya Tarafa yetu na ndipo kilipo kituo cha afya ambapo wanatibiwa wananchi wengi, hakuna mawasiliano. Je, Serikali ina mkakati gani kuweza kusaidia wananchi wetu ili hata mtu akiwa hospitali aweze kuwasiliana na ndugu zake?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ni upi mkakati wa Serikali ili kupunguza multiplicity ya minara kila sehemu? Kwamba, tuwe na mnara mmoja pengine na networks nyingine waweze ku-hire pale, ni upi mkakati wa Serikali katika jambo hili? (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwakiposa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, tunapokea ombi la Kata ya Kasanga ambayo, kama alivyoeleza mahitaji yake ni makubwa na kwa sababu ya huduma ambazo ziko pale. Nimuahidi kwamba, kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote tunazo kata na tunayo maeneo ambayo tutayapelekea huduma maalum. Nalichukua hili eneo na tutawaagiza watu wa UCSAF kwenda kufanya tathmini na kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023, tutajenga mnara kwenye eneo husika.

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Ni kweli kwamba, si jambo zuri kuwa na minara mingi katika mazingira tuliyonayo. Sisi Serikali kupitia Sheria ya EPOCA tunawahamasisha na kuwashawishi watoa huduma wachangie minara badala ya kila mtoa huduma kuwa na mnara wake. Changamoto iliyopo ni kwamba, baadhi ya maeneo na hasa ya vijijini ambayo watumiaji wa mtandao ni wachache, kiuchumi kuna changamoto ya ku-share mnara badala yake wana-opt kuachiana maeneo ili watoe huduma wasigawane wale watumia huduma wachache.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali tuko katika mchakato wa kuliwezesha Shirika letu la Mawasiliano - TTCL kumiliki minara na kwa sababu ni shirika la Serikali ni rahisi kuwabana wakawavutia wawekezaji watoa huduma wengine wakapanga kwenye minara ya TTCL badala ya ile ambayo inaendeshwa na watoa huduma ambayo kwa kweli, inaendeshwa kibiashara na inakuwa ngumu kwa maeneo ya vijijini ku-share kwa sababu ya gharama za uendeshaji. (Makofi)

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya mawasiliano katika Kata za Idete, Kiyowela, Maduma, Idunda, Makungu na Ihowanza?

Supplementary Question 2

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Jimbo la Mbinga Mjini, Kata ya Kitanda, Kikolo na Kagugu hakuna miundombinu ya mawasiliano. Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya mawasiliano ili kuwarahisishia wananchi kupata mawasiliano?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mbinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maeneo aliyoyataja naamini yako kwenye orodha ya kata ambazo mwaka ujao wa fedha tunapeleka minara ya simu, lakini kama kata zote hazikuingia kama nilivyosema, baadhi ya hizo kata zitakuwa zimeingia, zilizobaki tuko tayari kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kufanya tathmini ya mahitaji yaliyopo, tuangalie uwezo wa bajeti yetu hasa kwenye maeneo yale ambayo yanahitaji huduma maalum na tutafikiria kuona namna ya kupeleka huduma kwenye maeneo aliyoyataja.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya mawasiliano katika Kata za Idete, Kiyowela, Maduma, Idunda, Makungu na Ihowanza?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Awali ya yote niishukuru Wizara hii kwa kuwezesha mawasiliano katika Kata ya Likawage, Jimbo la Kilwa Kusini. Swali langu, ni nini mpango wa Serikali kupitia Wizara hii kuhakikisha kwamba, Kata za Nanjilinji, Kikole pamoja na Limalyao na zenyewe zinapata mawasiliano ya uhakika?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kata alizozitaja na ni kweli katika Wilaya na majimbo ambayo hali yake ya mawasiliano ni ngumu ni pamoja na Jimbo la Kilwa Kusini. Baadhi ya minara ambayo imejengwa ipo, lakini haijakamilika, ikikamilika itapunguza tatizo tulilonalo, lakini bila shaka Mheshimiwa Mbunge atakumbuka kwenye bajeti ya mwaka huu tumeweka zaidi ya minara mipya 700 nchi nzima, kwa hiyo, naamini kwamba, baadhi ya kata zake zitakuwemo. Kata zitakazobaki, nimhakikishie kwamba, tutakwenda kuzimalizia kwa ule utaratibu wa maeneo maalum.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya mawasiliano katika Kata za Idete, Kiyowela, Maduma, Idunda, Makungu na Ihowanza?

Supplementary Question 4

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Vijiji vya Upendo, Kijiji cha Shoga pamoja na Sipa vina changamoto kubwa sana ya mawasiliano. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba, vijiji hivi vinaweza kupata mawasiliano katika mwaka wa fedha unaokuja?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwenye majibu niliyoanza nayo mwanzo, mwaka huu wa fedha tumetenga minara mingi kidogo, lakini kwa maana ya eneo maalum analotoka Mheshimiwa Mbunge kwa sababu ya shughuli za kiuchumi zilizopo kwenye eneo hili tunazipa kipaumbele cha pekee. Kama katika orodha yetu tuliyoitoa wakati wa bajeti hizi kata na maeneo aliyoyataja hayamo, basi na yenyewe tutayaingiza kwenye orodha ya yale maeneo maalum, kwa sababu ya shughuli nyingi za kiuchumi ambazo zinafanyika kwenye eneo lake na sisi tuko tayari kushirikiana kusaidia katika ujenzi wa uchumi wa kidigitali, kwa maana ya kwamba, ule uchumi unaofanyika kwenye eneo lake uingie katika mfumo wa jumla wa uchumi wa kidigitali.