Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya vituo vya polisi vya Ilongero, Ngamu, Ngimu, Msange na Mtinko katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mhehimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana kwa nafasi, pamoja na majibu yao ya Serikali lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; ni lini sasa fedha hizi ambazo amezitaja Mheshimiwa Waziri zitaletwa kwaajili ya kuboresha miundombinu ya vituo hivi vya polisi vya Mtinko na Ngamu pamoja na kujenga vile vingine vya Msange na Ngimu maana yake tayari maeneo yapo?

Swali la pili nataka nijue, Serikali sasa inamkakati gani wa kujenga kituo cha polisi cha hadhi ya Wilaya katika Mji wa Ilongero ambao unakuwa kwa kasi unawatu wengi, lakini pia na kwa sasa ni Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya kwa hiyo, unahitaji usalama, huduma na pamoja na kwamba kituo hicho sasa eneo hilo linanyumba za polisi? Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili nyongeza ya Mheshimiwa Ighondo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja lini fedha? Bahati nzuri tumeshafanya tathimini tumepata shilingi milioni 46.4 zinahitajika kwaajili ya kukamilisha ukarabati huo, lakini katika mwaka huu wa fedha kama tulivyosema tutaendelea kutoa fedha kwa awamu kulingana na upatikanaji wake. Niombe kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa mwaka ujao tunachukua commitment ya kuweka fedha hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mkakati wa kujenga kituo cha polisi cha hadhi ya Wilaya niseme tu kwamba Wizara pamoja na Serikali kwa ujumla kuhakikisha tunajenga kituo chenye hadhi ya wilaya kwenye Makao Makuu ya Wilaya sasa hii ni Wilaya ya Singida ambayo OCD anaofisi yake lakini tutakachoweza kufanya ni kuimarisha vituo vya polisi ngazi ya kata na tarafa ili viweze kutoa huduma stahiki kwa wananchi badala ya kila jimbo kuliwekea kituo cha polisi chenye hadhi ya Wilaya. Nashukuru.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya vituo vya polisi vya Ilongero, Ngamu, Ngimu, Msange na Mtinko katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi hii; kutokana na ongezeko la uhalifu katika machimbo ya Rubi yaliyopo Mandala na Longido Mbunge wa Jimbo akishirikiana na wananchi wa pale kwa juhudi zao binafsi wamejenga kituo cha polisi mpaka ngazi ya lenta.

Je, ni lini Serikali itawasaidia wananchi hawa ili kumailizia kituo hiki cha polisi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Zaytun kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Wizara kwamba pale ambapo wananchi watakuwa wamefanya juhudi na kujenga kufika kiwango chochote Serikali inaweza ikatoa fedha kukamilisha. Niombe tushirikiane na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo na Mheshimiwa Zaytun wakati wa ziara yetu katika mkoa huo tuweze kuona kiwango kilichofikiwa ili kupitia Mfuko wetu wa Tuzo na Tozo tuone kiwango cha fedha tunachoweza kutoa ili kukamilisha kituo hicho kama njia ya kuunga mkono juhudi za wananchi. Nashukuru.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya vituo vya polisi vya Ilongero, Ngamu, Ngimu, Msange na Mtinko katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa ongezeko ni kubwa sana la uhalifu katika Mji wa Makambako na kwa sababu Makambako kipolisi ni Wilaya na tunakituo kimoja. Ni lini Serikali sasa itaondoa adha hii kwa kujenga kituo kingine pale Majengo, pale Idofi, pale Maguvani ili kuwaondolea adha wananchi waishi kwa amani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Sanga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua Mji wa Makambako umekuwa kwa kasi, kuna ongezeko kubwa la watu na shughuli za kiuchumi ambako ni kivutio kwa wahalifu pia. Nimuahidi tu kama kituo kilichopo kwa sasa hakikidhi haja, tutafanya tathmini kwa kushirikiana na uongozi wa Wilaya na kuona namna gani tutahitaji kufanya kwa maana ya kupanua huduma za polisi katika eneo lake. (Makofi)

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya vituo vya polisi vya Ilongero, Ngamu, Ngimu, Msange na Mtinko katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Supplementary Question 4

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; Tarafa ya Gonja yenye kata nne na Tarafa ya Mambavunja yeye kata tano zote hizi zimekuwa hazina kituo cha polisi na kwa muda mrefu tumeomba mpaka wananchi wameweka nafasi za kwamba polisi wanaweza kuanzia pale na kuna sehemu za kujenga vituo vya polisi.

Je, lini Serikali itatusaidia kujenga vituo hivyo? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kaboyoka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua uwepo wa baadhi ya tarafa na kata zisizokuwa na vituo vya polisi na polisi wetu tunaowapanga mpaka kwenye ngazi ya kata wanatumia majengo ambayo huamuliwa na mamlaka zetu za Serikali za Mitaa. Nimuombe Mheshimiwa Kaboyoka kuwa na subira, tunavyoanza kutekeleza mkakati wetu wa kujenga vituo vya polisi mahala ambako hakuna kabisa vituo, zikiwemo tarafa alizozitaja huko Gonja. Nashukuru.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya vituo vya polisi vya Ilongero, Ngamu, Ngimu, Msange na Mtinko katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Supplementary Question 5

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kuuliza swali moja la nyongeza ambalo dogo tu.

Je, ni lini Serikali itaweka uzio katika Kituo cha Polisi cha Ng’ambo, Wilaya ya Mjini Unguja? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba uzio upo katika baadhi ya vituo vya polisi. Lakini niseme kwa kuwa baadhi ya maeneo hayana kabisa vituo vya polisi, kipaumbele hakiwezi kuwekwa kwenye uzio, kipaumbele cha Wizara ni kuweka vituo mahala ambako hakuna vituo kabisa na nyumba za makazi kwa ajili ya askari wetu. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa atuvumilie tumalize vipaumbele then haya mambo mengine ya uzio yafuate. Nashukuru.