Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa Vitambulisho vya NIDA kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma hususan Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, bado kwa takwimu Mkoa wa Kigoma una zaidi ya wananchi 2,000,000 lakini waliotambuliwa ni 975,844 na waliopata vitambulisho ni 123,962 sawa na asilimia 12 tu. Jibu lake anasema kwamba mwaka huu watapewa vitambulisho; sasa swali nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wote wanaostahili ambao wako katika Mkoa wa Kigoma wanapata vitambulisho vya NIDA?

Mheshimiwa Spika, la pili; wananchi wa Wilaya ya Kakonko muda mwingine wanaombwa vitambulisho ambavyo ni vya NIDA ambavyo hakika Serikali inajua kwamba haijavitoa kwa wananchi hao, mpango ukoje kuhakikisha kwamba wananchi wa Wilaya ya Kokonko sasa wanapata vitambulisho vya NIDA? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kamamba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kwa takwimu hizo idadi ya waliopata vitambulisho ni ndogo sana, lakini kama ilivyoelezwa wakati nawasilisha bajeti hapa kulikuwa na changamoto ya kimkataba kati ya Serikali na mzabuni, na hivyo karatasi za kutolea vitambulisho hivi hazikuwepo, lakini tatizo hilo limeondolewa, tumeshahuisha mkataba na ndio maana tunauhakika kwamba kwa mwaka ujao wa fedha tutatatua tatizo hilo kwa wale wote waliotambuliwa na kusajiliwa na wale wapya tutakaokuwa tunaweza kutawambua na kuwasajili, nashukuru kwa swali la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kuhusu kugawa vitambulisho kama nilivyosema kwenye jibu la msingi linahusiana moja kwa moja kwa mwaka ujao tunauhakika wananchi wale ambao wameshatambuliwa watapewa vitambulisho na wale wapya watakaokuwa wanaendelea kutambuliwa watapewa vitambulisho, nashukuru.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa Vitambulisho vya NIDA kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma hususan Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; kwa kuwa kuwa na kitambulisho cha Taifa ni haki ya kila Mtanzania, je, ni nini kauli ya Serikali kwa wafungwa na maabusu wa muda mrefu juu ya kupatiwa huduma hii?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ni haki la kila raia kupata kitambulisho, lakini kwa hawa ambao wamefungwa sidhani kama kuna dharura ya kiasi hicho, kwa sababu hawa wapo jela vitambulisho vinatakiwa kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali ikiwemo elimu, mikopo, safari, passport na kadhalika, sasa huyu mfungwa tuhangaike kumpa kitambulisho anakwenda kukitumia wapi. Lakini tuahidi atakapokuwa amemaliza kifungo chake akirudi uraiani atatambuliwa na kupewa kitambulisho kama inavyopaswa, nashukuru. (Makofi)

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa Vitambulisho vya NIDA kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma hususan Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 3

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; moja ya changamoto ambayo inayopelekea kuchelewa kuwapa vitambulisho vya NIDA wananchi wa Mkoa wa Mtwara ni pamoja na uhaba wa watumishi; je, Serikali imejipanga vipi kuondoa changamoto hii? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anastazia Wambura kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu ya maswali yaliyopita, kwa kweli changamoto sio idadi ya watumishi changamoto ilikuwa ni kukosa vitendea kazi vilivyokuwa vimesababishwa na kukwama kwa mkataba, sasa baada ya suala la mkataba tumeshalitatua bila shaka ataona kasi ya utoaji wa vitambulisho kule Mtwara inatatuliwa, lakini pale itakapoonekana kwamba shida ni watumishi Serikali itaendelea kuajiri watumishi wanaohitajika ili kutekeleza majukumu yako ya utoaji wa vitambulisho itasavyo.