Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami inayounganisha Mji Mdogo wa Mtowisa na Sumbawanga Mjini kupitia Mlima Ng’ongo?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii ya maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nishukuru na kuipongeza Serikali kutenga hiyo fedha ambayo itakuwa na matumaini makubwa kwa wananchi wa Mtowiso wanaosubiri barabara hiyo ya Ng’ongo.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza la nyongeza; kwa kuwa Serikali mmetumia shilingi milioni 900 kujenga barabara ya Msia - Mawezuzi, kwenda Sumbawanga Mjini na bado haijakamilika.

Je, ni lini mtaleta shilingi bilioni 1.5 zilizobaki ili kukamilisha barabara hii ipitike?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili la nyongeza; kutokana na mvua nyingi mwaka huu barabara za Kijiji cha Kamsamba ambayo inaunganisha Kijiji cha Kavifuti na Miangalua ilibebwa na maji na mpaka sasa tumeandika andiko liko Wizarani. Nataka kujua je, ni lini fedha hizo za dharura zitakuja ili kutengeneza Daraja hilo la Kamsamba?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali ilikuwa imetoa fedha milioni 900 na mpaka sasa tunahitaji kuongezea fedha ambapo ziko katika mchakato na mchakato ukikamilika fedha ile itapelekwa ili barabara hiyo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameianisha hapa iweze kumalizia hicho kipande kilichobakia.

Mheshimiwa Spika, lakini suala la pili, wameomba fedha kwa ajili ya barabara ambayo imeharibika kutokana na mvua na fedha hizo ni za dharura, na ni kweli hilo andiko lipo Ofisi ya Rais, TAMISEMI (TARURA) na sisi tuko katika hatua za mwisho kuhakikisha kwamba hiyo fedha tunaipata ili tulete na turekebishe barabara hiyo, kwa hiyo, hayo ndiyo majibu.