Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga mradi wa maji wa vijiji tisa vya Kata za Oldonyosambu na Oldonyowas?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimia Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa mradi huo umechukua muda mrefu na sasa wananchi wanakunywa maji ya floride na wanazaliwa watoto wenye vichwa vikubwa, vibiongo na miguu kupinda. Je, Serikali haioni sasa kufanya haraka kwa ajili ya kukamilisha mradi huo?

Swali la pili, je, Naibu Waziri wa Maji baada ya Bunge hili atakuwa tayari kwenda kukagua mradi huo ili kujionea hali halisi ya wale wananchi wanavyoteseka?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Saputu kama ifuatavyo;-

Mheshimiwa Naibu Spika, huu mradi tumeweka nguvu kubwa lakini tumekusikia Mheshimiwa Mbunge tutaongeza nguvu.

Swali la pili kukagua mradi mara baada ya Bunge hili Mheshimiwa Mbunge unafahamu nilishakuja Jimboni kwako hivyo sitasita kufika tena kuhakikisha huduma ya maji inapatikana.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga mradi wa maji wa vijiji tisa vya Kata za Oldonyosambu na Oldonyowas?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; Mheshimiwa Waziri Engineer rafiki yangu nadhani wananchi wa Nyatwali nilikukutanisha nao kata yao wana mradi mkubwa umekamilika na wamekuambia huo mradi haujazinduliwa, kigugumizi cha kuzindua huo mradi ni kitu gani?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya kama ifuatavyo:-

Ni kweli Mheshimiwa Ester tulikutana na wale madiwani na wananchi wa ile kata nilikubali nitakuja tusubiri Bunge liishe tutafika na litazinduliwa kwa sababu tunahitaji wananchi wapate maji.