Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 261 2022-05-25

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:-

Je, ni nini mpango wa Serikali kufanya asilimia 50 ya wanafunzi wanaojiunga na Kidato cha Tano katika shule za Kata watoke ndani ya Halmashauri?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la Serikali kuchanganya wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali ili kujenga Utaifa, kuchanganya wanafunzi kunasaidia msawazo wa nafasi zilizopo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa wanafunzi wote waliofaulu wanapata nafasi ya kujiunga Kidato cha Tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutumia wanafunzi asilimia 50 kujiunga na Shule za Sekondari kutasababisha baadhi yao kukosa nafasi kwa kuwa siyo kila mchepuo unapatikana kwenye shule zilizopo katika Halmashauri husika.