Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 260 2022-05-25

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Afya katika Kijiji cha Mikuwa Kata ya Mnanje Wilayani Nanyumbu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepeleka fedha Shilingi Milioni 250 kwenye Kata ya Mnanje kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya ambapo Kijiji cha Mikuwa ni miongoni mwa vijiji vilivyomo kwenye Kata hiyo. Majengo yanayojengwa kwenye Kituo hicho ni jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje (OPD), Jengo la maabara na kichomea taka. Majengo hayo yapo katika hatua ya umaliziaji ukiacha kichomea taka ambacho ujenzi wake ndiyo umeanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais – TAMISEMI tayari imekwisha wasilisha maombi Wizara ya Fedha na Mipango ya Shilingi Milioni 250 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa wodi ya wazazi, chumba cha upasuaji na jengo la kufulia.