Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 25 Water and Irrigation Wizara ya Maji 223 2022-05-18

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha matengenezo ya miundombinu ya usambazaji maji katika kata sita za Muheza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamis Mohamed Mwinjuma, Mbunge wa Jimbo la Muheza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka 2021/2022 inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya maji katika kata sita za Muheza ambazo ni Mbaramo, Genge, Masuguru, Tanganyika, Majengo na Kwemkabala. Ukarabati huo unahusisha kazi ya kubadilisha bomba kuu lenye urefu wa kilomita Mbili na ukarabati wa bomba la usambazaji maji lenye urefu wa kilomita 14.5. Kazi hii itakamilika mwezi Oktoba, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali imepanga kuendelea na ukarabati wa miundombinu katika Kata Sita za Mji wa Muheza ikiwa ni pamoja na kusambaza maji katika maeneo ambapo mtandao wa usambazaji maji haujafika kwenye Kata hizo.