Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 53 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 697 2023-06-22

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka Gari la Wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Mlola Wilayani Lushoto?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Jimbo la Lushoto, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mahitaji ya kuwa na magari ya wagonjwa kwenye Vituo vya Afya na Hospitali ili kurahisisha huduma za rufaa kwa wagonjwa. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali imetenga shilingi bilioni 35.1 kwa ajili ya ununuzi wa magari 316 ya kubebea wagonjwa.

Mheshimiwa Spika, magari haya yameanza kupokelewa kwa awamu na yatagawiwa katika Halmashauri zote nchini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ambayo itapata magari mawili kwa ajili ya huduma za rufaa za wagonjwa.