Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 717 2023-06-23

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:-

Je, Mwaka 2021 – Januari, 2022 Sekta ya Mifugo imeuza nyama nje ya nchi kwa asilimia ngapi na upi mkakati wa kuimarisha Sekta hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya tani 10,415 za nyama zimeuzwa nje ya nchi zenye thamani ya dola za Kimarekani 42,500,994.90 ikilinganishwa na tani 1,774.29 za nyama zenye thamani ya dola za Kimarekani 4,290,000 zilizouzwa katika mwaka wa fedha 2020/2021. Ongezeko hili ni sawa na asilimia 492.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na mikakati mbalimbali ya kuimarisha tasnia ya nyama ikiwemo; kuvutia uwekezaji katika ujenzi wa machinjio za kisasa zinazokidhi viwango vya kimataifa ambapo hadi sasa, zipo machinjio sita tu zenye ithibati ya kuuza nyama nje ya nchi; kuimarisha mazingira ya ufanyaji biashara katika tasnia ya nyama kwa kupunguza tozo na kodi za usafirishaji wa nyama nje ya nchi; kuwajengea uwezo vijana waliohitimu vyuo vya mifugo kupitia vituo atamizi ili waweze kufuga kisasa na kuzalisha malighafi ya kutosha kwa ajili ya viwanda vya kuchakata nyama na kuboresha mbari za mifugo kupitia uhimilishaji, ugawaji wa madume bora na usambazaji wa mitamba ya ng’ombe wa nyama.