Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 710 2023-06-23

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutokomeza kabisa ugonjwa wa Malaria nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bernadeta Kasabago, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza afua kuu zifuatazo katika kutokomeza ugonjwa wa Malaria: -

(i) Udhibiti wa mbu waenezao Malaria kupitia njia kuu zifuatazo:-

(a) Kusambaza vyandarua vyenye dawa kwa jamii kupitia kampeni za kugawa vyandarua kwa kila kaya; kliniki za mama wajawazito, watoto na vituo vya kutolea huduma kwa makundi maalum kama wazee.

(b) Upuliziaji wa dawa ukoko kwenye kuta ndani ya nyumba katika maeneo yenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya malaria.

(c) Unyunyiziaji wa viuadudu vya kibaiolojia kwenye mazalia ili kuuwa viluilui wa mbu.

(ii) Kuhakikisha vipimo na dawa za malaria zinapatikana wakati wote katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini. Vipimo na dawa za Malaria zinapatikana bila malipo kwenye vituo vyote vya kutolea huduma vya Serikali.

(iii) Kuhamasisha jamii kutumia njia mbalimbali za kujikinga na ugonjwa wa malaria.

Mheshimiwa Spika, ili kuharakisha kufikiwa kwa azma ya kutokomeza ugonjwa wa malaria hapa nchini, Serikali imeanzisha Baraza la Kutokomeza Malaria (End Malaria Council) lililozinduliwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu tarehe 25 Aprili, 2023. Ahsante.