Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 733 2023-06-26

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuvutia Wawekezaji wa Viwanda vya kuchakata Madini ya chumvi Wilayani Kilwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkakati wa Serikali kuvutia wawekezaji katika sekta ya Chumvi unaendelea ikiwa ni pamoja na kutenga eneo lenye ukubwa wa hekta 168 katika Wilaya ya Kilwa kwa ajili ya wawekezaji wenye nia ya kuchakata madini ya chumvi.

Mheshimiwa Spika, Aidha, Serikali imeendelea kutoa vivutio mbalimbali vya kikodi na visivyo vya kikodi kwa uratibu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Taasisi husika ili kufanikisha azma ya kuwekeza katika sekta husika kwa maana ya sekta ya madini.