Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 731 2023-06-26

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, lini mgogoro wa ardhi wa Shamba la Kambenga utatatuliwa?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Kijiji cha Namwawala ilimpatia Ndugu Kassim Seif Kambenga ardhi yenye ukubwa wa ekari 1,000 mwaka 1989. Mgogoro uliibuka miaka ya 2000 baada ya Serikali ya Kijiji cha Namwawala kugawa ekari 900 kati ya 1,000 kwa wananchi wengine kutokana na ndugu Kambenga kufanya upimaji wa awali na kukamilisha umilikishwaji wa ekari 100 tu. Mgogoro huu ulifikishwa kwenye vyombo vya sheria hususan Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya kupitia Shauri Na. 2/2007 na Mahakama Kuu (Kitengo cha Ardhi) kupitia Shauri Na. 2/2012 ambapo Kassim Seif Kambenga alipewa ushindi kuwa ni mmiliki halali wa shamba lenye ekari 1,000.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia mahitaji ya ardhi ya wananchi wanaozunguka shamba hilo, Serikali kupitia uongozi wa Wilaya na Mkoa inaendelea na mazungumzo na familia ya ndugu Kassim Seif Kambenga ili akubali kumega kiasi cha shamba lake kwa ajili ya kuwapatia wananchi. Hivyo, wananchi wanaombwa kuwa na subira wakati Serikali inapoendelea kushughulikia suala hili.