Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Water and Irrigation Wizara ya Maji 730 2023-06-26

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, mchakato wa mradi wa kutoa maji Ziwa Tanganyika umefikia wapi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika kuwapatia wananchi wa Mkoa wa Rukwa huduma ya majisafi na salama. Usanifu kwa ajili ya kuwapatia wananchi maji katika vijiji 40 vya pembezoni mwa ziwa umekamilika na tayari wananchi kwenye vijiji tisa wanapata maji na miradi inaendelea kutekelezwa kwenye Vijiji vilivyobaki hatua kwa hatua. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itaajiri mtaalam mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu wa miradi ya maji kupitia chanzo cha Ziwa Tanganyika ili kunufaisha maeneo mengi zaidi Mkoani Rukwa.