Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 727 2023-06-26

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi wa Magari cha Muhalala – Manyoni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Kituo cha Ukaguzi wa Pamoja cha Muhalala Manyoni ulisimama kutokana na mkandarasi kusitisha utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kituo hicho tarehe 11 Septemba, 2018 ukiwa umefikia 60.1%.

Mheshimiwa Spika, kusitishwa kwa ujenzi wa mradi huo kulisababisha mkandarasi kuingia katika mgogoro wa kimkataba na Serikali. Hivi sasa Serikali iko katika hatua ya kukamilisha makubaliano ya stahili za pande zote mbili kati ya Serikali na mkandarasi. Aidha, kwa kuwa Mkataba wa Ufadhili chini ya Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) bado unaendelea, Serikali itaendelea na mchakato wa kutafuta mkandarasi mwingine atakayemalizia kazi zilizobaki mara baada ya makubaliano ya stahili kukamilika, ahsante.