Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 726 2023-06-26

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, lini Serikali italipa fidia kwa maeneo ya Kahe/Chekereni na Njiapanda yaliyochukuliwa na TANROADS mwaka 2013?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwaka 2015 Serikali ilifanya na kukamilisha uthamini kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi 146 watakaoathirika na ujenzi wa mradi wa vituo vya ukaguzi wa pamoja wa magari ya mzigo (One Stop Inspection Station) ambapo kiasi cha shilingi bilioni 5.048 kilihitajika kuwalipa waathirika hao lakini hawakulipwa kutokana na Sheria Na. 7 ya Mwaka 2016 ya Uthamini na Usajili.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANROADS Mkoa wa Kilimanjaro, inarudia zoezi la uthamini ulioanza tarehe 10 Mei, 2023 ambapo zoezi hilo lipo kwenye hatua za mwisho kukamilika. Baada ya zoezi hilo kukamilika waathirika watalipwa fidia zao, ahsante.