Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 724 2023-06-26

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza:-

Je, Serikali inachukua hatua gani kwa uvamizi wa tembo kwa wananchi na mashamba katika Wilaya za Liwale na Nachingwea?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inakiri kuwepo na changamoto ya wanyama wakali na waharibifu wakiwemo tembo. Kwa sasa Serikali inaendelea kutekeleza mkakati wa kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu wa mwaka 2020 – 2024. Wizara inaendelea kufanya yafuatayo; kutoa elimu juu ya kujikinga na wanyamapori wakali na waharibifu; kujenga vituo vya askari wanyamapori ili kusogeza huduma karibu na wananchi; kuwafunga mikanda tembo na kuanzisha timu maalum (rapid response teams).

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuwashirikisha wananchi kwa kutoa mafunzo kwa Askari wa Vijiji (VGS) ili kuongeza nguvu ya kudhibiti tembo katika maeneo ya wananchi. (Makofi)