Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 759 2023-06-28

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza kilimo cha minazi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha kilimo cha minazi nchini ambapo imeanzisha shamba lenye ukubwa wa hekta 54 katika Kituo Kidogo cha Utafiti cha Chambezi, Wilaya ya Bagamoyo ili kuzalisha miche iliyo bora ya minazi. Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imepanga kuzalisha miche bora 750,000 na kuisambaza kwa wakulima wa zao la minazi ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo na kuanzisha mashamba makubwa ya pamoja.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali imeanza mazungumzo na Kampuni ya Deejay Coconut Farm Private Ltd. ya nchini India katika mashirikiano ya uzalishaji wa miche ya inayozalisha nazi 250 kwa mnazi mmoja kulinganisha na minazi ya kawaida inayozalisha nazi 80 kwa mti mmoja.