Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 689 2023-06-21

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kufufua zao la kahawa nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ya kufufua zao la kahawa hususan katika maeneo yenye mibuni iliyozeeka, mashamba yaliyotelekezwa na kuanzisha kilimo cha kahawa katika maeneo mapya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati hiyo inajumuisha uzalishaji na usambazaji wa miche bora ya kahawa; kuimarisha maabara za kuzalisha miche kwa njia ya chupa ili kudhibiti magonjwa na kuongeza kasi ya uzalishaji wa miche bora; kuboresha mifumo ya masoko ya kahawa ili kumlinda mkulima; kuwezesha matumizi ya teknolojia za umwagiliaji kwenye mashamba ya kahawa na kuimarisha utafiti na maendeleo kupitia Kituo cha Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI).

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika msimu wa mwaka 2022/2023 jumla ya miche 8,784,146 ilizalishwa na kusambazwa kwa wakulima. Kati ya kiasi hicho, miche 5,458,123 ni aina ya arabika na miche 3,326,023 ni aina ya robusta. Aidha, katika mwaka 2023/2024 Serikali imepanga kuanzisha mashamba 40 ya mfano katika wilaya 20, kuratibu uzalishaji na usambazaji wa miche bora 20,000,000 katika wilaya 52 na kufufua mashamba 150 yenye jumla ya hekta 400.