Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 686 2023-06-21

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani – Nalasi hadi Tunduru utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) tayari imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara ya Mtwara Pachani – Nalasi hadi Tunduru yenye urefu wa kilometa 300. Katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali imepanga kuendelea na ujenzi wa kilometa mbili katika Mji wa Tunduru. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa sehemu iliyobaki, ahsante.