Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 629 2023-06-14

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Nduguti kwa kuwa ujenzi wake umesimama kwa muda mrefu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi Wilaya ya Mkalama ambacho kinajengwa eneo la Nduguti ni kituo cha Daraja B na ujenzi wake ulisimama ukiwa umefikia hatua ya lenta. Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023 ilitenga kiasi cha fedha shilingi 500,000,000 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa kituo hicho. Mwezi Februari, 2023 Serikali ilitoa shilingi 300,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.