Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 627 2023-06-14

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa KV 400 kutoka Iringa, Mbeya, Tunduma hadi Sumbawanga utaanza pamoja na kulipa wananchi waliopitiwa na laini hiyo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa KV 400 yenye urefu wa kilometa 620 kutoka Iringa hadi Sumbawanga kupitia Mbeya na Tunduma unatarajiwa kuanza mwezi Juni, 2023 na kukamilika mwezi Septemba, 2025. Mradi huu unalenga kuunganisha Gridi ya Taifa na Nchi za Kusini mwa Afrika (Southern African Power Pool) na utagharimu jumla ya shilingi 1,380,000,000,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari imetoa shilingi bilioni 16.43 kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wananchi 6,500 wanaopisha mradi na kazi ya ulipaji fidia imekamilika kwa awamu ya kwanza ambapo wananchi 4,750 wamepokea shilingi bilioni 13.67 na maandalizi ya awamu ya pili yanaendelea na malipo yanatarajiwa kufanyika ifikapo Julai, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.