Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 620 2023-06-14

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga barabara ya Ninde, Masokolo hadi Lupata katika Kata ya Kuzumbi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Ninde – Masokolo – Lupata yenye urefu wa kilometa 40 inahudumia vijiji vitatu ambavyo ni Ninde, Masokolo na Lupata. Barabara hii ipo mpakani mwa Tanzania na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo ni muhimu kwa shughuli za kufuatilia masuala ya kiusalama. Barabara hii haipo kwenye mtandao wa barabara za TARURA. Hivyo, barabara hiyo inahitaji kufunguliwa ili kuunganisha vijiji hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itafungua barabara hii kulingana na upatikanaji wa fedha ili kuimarisha usafiri na usafirishaji.