Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 43 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 564 2023-06-08

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: -

Je, ajali ngapi za barabarani zimetokea kati ya Mikumi na Ruaha Mbuyuni kwa Mwaka 2010 hadi 2022?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi 2022 ajali za barabarani zilizosababishwa na vyombo vya moto katika eneo la Mikumi hadi Ruaha Mbuyuni, barabara ya Morogoro kwenda Iringa ni 128. Mchanganuo wa ajali hizo ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ajali zilizohusisha mabasi ya abiria ni 30, malori 42 na magari madogo 56, nashukuru.