Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 562 2023-06-08

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: -

Je, Serikali inawasaidiaje Wanafunzi wenye mahitaji maalum katika huduma za vyoo kwenye shule za msingi na sekondari nchini?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali lililoulizwa na Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiboresha ramani za ujenzi kwa shule za msingi na sekondari ili kukidhi mahitaji ya makundi maalum ya wanafunzi. Kwa sasa Serikali imeelekeza kwamba kila panapojengwa matundu ya vyoo lazima kuhakikisha kwamba mahitaji ya watu wenye mahitaji maalumu nayo yanaangaliwa.

Mheshimiwa Spika, Maelekezo yalishatolewa kwa viongozi wa ngazi mbalimbali ikiwemo Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa kuwa ujenzi wa shule mpya, ujenzi wa matundu ya vyoo uzingatie ramani ilyotolewa tarehe 20 Februari, 2023, ambayo ndani yake mahitaji ya watu maalum yameangaliwa.