Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 552 2023-06-07

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza:-

Je, lini wananchi waliopitiwa na ujenzi wa Bwawa la Umeme la Mto Lumakali Makete watalipwa fidia?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa ujenzi wa Bwawa la Mto Lumakali unalenga kuzalisha umeme wa MW 222 kwa kutumia maji ya Mto Lumakali mkoani Njombe na unahusisha pia ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme yenye msongo wa kV 220 yenye urefu wa kilometa 65 kutoka kwenye mitambo hadi Kituo cha Kupoza Umeme cha Iganjo mkoani Mbeya. Gharama za ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme ni takribani shilingi trilioni 1.42 na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ni takribani shilingi bilioni 50.3.

Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini ya awali ya mali za wananchi wanaopisha Mradi wa Ujenzi Bwawa la Umeme la Mto Lumakali imekamilika na Serikali imetenga fedha katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya kuanza malipo ya fidia kwa wananchi hao. Kwa sasa kazi ya uhakiki inaendelea kwa mwezi Juni, 2023 na baada ya kazi hiyo kukamilika malipo ya fidia kwa wananchi wanaopisha mradi yanatarajiwa kuanza kulipwa kuanzia mwezi Julai, 2023, nashukuru.