Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 545 2023-06-07

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaupa hadhi ya Manispaa Mji wa Kibaha ambao ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silyvestry Francis Koka, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, halmashauri huanzishwa au kupandishwa hadhi kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa Sura ya 287 na 288 pamoja na Mwongozo wa uanzishwaji wa Maeneo ya Utawala wa mwaka 2014 ambapo umeainisha vigezo na taratibu zinazopaswa kufuatwa ili kuanzisha na kupandisha hadhi halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, Aprili, 2023 Halmashauri ya Mji Kibaha iliwasilisha ombi la kupandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Manispaa. Maombi haya yamepokelewa na yatafanyiwa kazi kwa kuzingatia vigezo vilivyopo.