Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 526 2023-06-05

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua skimu ya umwagiliaji katika Kijiji cha Mtitaa Wilayani Bahi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Nollo, Mbunge wa Jimbo la Bahi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Skimu ya Umwagiliaji Mtitaa iliyopo katika Kijiji cha Mtitaa, Kata ya Mtitaa Wilayani Bahi, ilijengwa kupitia Mpango Shirikishi wa Kuendeleza Kilimo cha Umwagiliaji (PIDP) katika mwaka wa fedha 2002/2003 na kuanza uzalishaji mwaka 2003/2004. Skimu hii pia ina miundombinu ya bwawa dogo la kuvuna maji msimu wa mvua na zao linalolimwa ni Mpunga. Skimu ina jumla ya hekta 107 na ina jumla ya wakulima 215.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imetenga fedha za ukarabati wa skimu za Bonde la Bahi ikiwemo skimu ya Mtitaa ambazo zimeharibiwa na mafuriko ili kuzirudisha kwenye uzalishaji.