Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 525 2023-06-05

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha Vijiji vyote vya Mkoa wa Songwe vinapatiwa umeme wa REA?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Songwe una jumla ya vijiji 307 ambapo hadi kufikia tarehe 31 Mei 2023, vijiji 240 vilikua tayari vimepatiwa umeme, Vijiji 67 vilivyosalia viko kwenye mkataba wa Mkandarasi M/s Derm Electrics Ltd anayetekeleza mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu III Mzunguko wa II katika Mkoa wa Songwe. Kazi za ujenzi wa miundombinu na kuunganisha wateja katika vijiji hivyo inaendelea na mradi unatarajiwa kukamilika Desemba, 2023, nakushukuru.