Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 520 2023-06-05

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-

Je, kwa nini viongozi wastaafu wa vitongoji na vijiji wenye sifa siyo wanufaika wa TASAF?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa uratibu wa awamu ya kwanza ya mpango wa kunusuru walengwa wa kaya maskini ulipoanza, taratibu zilibainisha kuondoa baadhi ya makundi wakiwemo watumishi wastaafu wanaopokea pensheni, watu walioajiriwa na kuwa na kipato cha uhakika, Viongozi wa Vijiji na Wajumbe wa Kamati za Usimamizi za Jamii miongoni mwao ni Viongozi wa CCM katika ngazi za Kata na vijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia maboresho ya taratibu za utambuzi na uandikishaji wa walengwa ya mwaka 2021, Kaya za Viongozi wa kisiasa wakiwemo Mabalozi wa Nyumba Kumi na Viongozi waliopo na wastaafu wa vijiji na vitongoji zinazokidhi vigezo zilipewa fursa ya kutambuliwa na kuandikishwa kwenye mpango huo wakati wa zoezi la utambuzi na uandikishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa rai kwa viongozi wastaafu wa vijiji na vitongoji ambao kipindi cha zoezi la utambuzi wa walengwa linafanyika walikubalika na jamii kuorodheshwa awali kuwa katika kaya maskini wajiandishe ili nao waweze kuingia katika mpango huo.