Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 497 2023-06-01

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kubadilisha utaratibu wa utoaji vibali vya kuvuna miti ili kuhusisha Kamati za Maendeleo za Kata na Vijiji?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, usimamizi na matumizi ya rasilimali za misitu hufanywa kwa mujibu wa Sheria ya Misitu Sura 323 na Kanuni zake za mwaka 2004. Aidha, katika kuhakikisha matumizi endelevu, Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii huandaa mwongozo unaotoa namna ya kutoa vibali na usimamizi wa jumla wa matumizi ya misitu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia utaratibu huo Serikali ilitoa mwongozo mwaka 2017 unaofahamika kama ‘Mwongozo wa Uvunaji Endelevu wa Mazao ya Misitu.’ Mwongozo huo umebainisha wajumbe wanaounda kamati ya uvunaji ngazi ya wilaya chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Wilaya.