Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 465 2023-05-29

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanzisha Vituo Maalum vya Masuala ya Uwekezaji na Masoko kwa Wanawake katika kila Kata?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji nchini kwa ajili ya wazawa na wageni wakiwemo wanawake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanzisha majukwaa ya kiuchumi mahususi kwa ajili ya wanawake. Majukwa haya yanatoa fursa kwa ajili ya wanawake kuona fursa za uwekezaji na biashara na kuzitumia ikiwemo masoko ya bidhaa wanazozalisha. Aidha, Serikali imeendelea kutambua kundi la wanawake na kuwapa fursa ya kukopeshwa mikopo mbalimbali ikiwemo mikopo ya 10% kutoka kwenye halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuangalia fursa mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha wanawake na pale itakapoonekana kuna haja ya kuanzisha vituo vya uwekezaji wa masoko mahususi kwa wanawake, basi kazi hiyo itafanyika katika ngazi ya kata, nashukuru.