Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 138 2023-09-08

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi kwa kumalizia ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Itumbi na Kambikatoto, Lupa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Vituo vya Polisi vya Itumbi na Kambikatoto ni vituo vinavyojengwa kwa nguvu za wananchi na mpaka kumalizika ujenzi wake vitagharimu kiasi cha fedha shilingi 279,780,978. Fedha inayohitajika ili kumalizia ujenzi kwa kuunga mkono nguvu za wananchi, ni shilingi 173,447,178. Fedha hizo zitatoka kwenye Mfuko wa Tuzo na Tozo kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ili kumalizia ujenzi huo kama njia ya kuwaunga mkono wananchi wa Jimbo la Lupa.