Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 133 2023-09-08

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kujenga kivuko cha juu barabara ya njia nane eneo la Magari Saba Mbezi ili kulinda uhai wa wananchi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Kibamba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, eneo la Magari Saba, eneo la Mbezi, limekwishawekwa kivuko cha pundamilia (zebra crossing) kwa wapita kwa miguu ili kuwawezesha watumiaji wa barabara hiyo kuvuka kwa usalama katika eneo hilo, ahsante.